Jumatano, 13 Juni 2018

NAIBU WAZIRI WA ELIMU ASEMA SERIKALI HAITAFUMBIA MACHO VITENDO VYA UDHALILISHAJI DHIDI YA WANAFUNZI


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mheshimiwa William Ole Nasha amesema Serikali haitafumbia macho vitendo vya udhalilishaji dhidi ya wanafunzi na kuwa Sheria kali zitachukuliwa kwa wale wote watakaobainika kuhusika na vitendo hivyo.

Naibu Waziri Ole Nasha ametoa kauli hiyo leo Mkoani Dodoma wakati wa mahojiano maalumu na Shirika la Utabgazaji la Taifa - TBC ambapo amesema Sheria za nchi ziko wazi kwa mtu yeyote atakaebainika kufanya vitendo vya ngoni basi adhabu yake ni miaka 15 jela hadi kifungo cha maisha.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mheshimiwa William Ole Nasha akifanya mahojiano na mtangazaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania-TBC wakati huu ambapo Mataifa mbalimbali yakijielekeza katika kudhimisha siku ya mtoto wa Afrika. Mahojiano hayo yamefanyika Jijini Dodoma ambapo Naibu Waziri ameelezea pia mafanikio mbalimbali kuhusu sekta ya Elimu. 

Mheshimiwa Ole Nasha pia ameitaka Idara ya Uthibiti Ubora wa Shule nchini kuhakikisha unafanya ufuatiliaji kwa lengo la kuhakikisha Elimu bora inapatikana nchini kwa kuwa hilo ndiyo jukumu lao.

“Kuna maeneo bado Idara ya uthibiti ubora haijafanya vizuri, mfano katika hili tukio la St. Florence Idara hiyo ina kitu cha kujibu,” licha ya kuwa vyombo vingine vya Sheria vinaendelea na uchunguzi lakini na sisi ndani ya Wizara tunafanya uchunguzi kuona nani kazembea katika suala hilo,” alisisitiza Naibu Waziri Ole Nasha.

Naibu Waziri pia amewataka wazazi kuhakikisha watoto wote waliofika umri wa kwenda shule wanakwenda shule kwa kuwa hivi sasa Elimu msingi kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha Nne inatolewa bure.

Akizungumzia kuhusu viwanda Mheshimiwa Ole Nasha amesema vyuo vya ufundi ndiyo njia sahihi ya kulipeleka Taifa katika Uchumi wa Kati, hivyo kupitia vyuo hivyo Taifa litapata  nguvukazi na  sahihi ambayo itatumika kwenye viwanda.


Ijumaa, 8 Juni 2018

SERIKALI YASEMA HAITAVUMILIA WALIMU WANAOSHIRIKI VITENDO VYA UDHALILISHAJI KWA WANAFUNZI


Serikali imesema haitavumilia vitendo vya udhalilishaji ambavyo vimekuwa vikijitokeza katika baadhi ya shule hapa nchini na kusisitiza kuwa hatua kali za kisheria zitachukukuliwa kwa wale wote watakaobainika kuhusika na vitendo hivyo.

Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako mkoani Dodoma wakati akikabidhi tuzo kwa wanafunzi waliofanya vizuri kitaifa katika masomo yao ya kuhitimu darasa la saba, Kidato Cha Nne na kidato Cha Sita kwa shule za serikali na zisizokuwa za serikali.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akitoa cheti na fedha kwa mwanafunzi bora kitaifa katika masomo ya sayansi Sophia Juma  aliyefanya vizuri katika matokeo ya kumaliza kidato cha sita mwaka 2017. Utoaji wa tuzo hizo umefanyika mkoani Dodoma katika kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Elimu

Waziri Ndalichako amewataka wanafunzi nchini kote kusoma kwa bidii, kuwa na nidhamu pamoja na kuishi kwa kufuata maadili ya kitanzania na siyo kuiga maadili ya watu wa nje.

“Wakuu wa shule nchini kote nawaagiza kuhakikisha mnasimamia kwa weledi malezi ya wanafunzi, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha walimu mnakemea vitendo vya udhalilishaji ambavyo vimekuwa vikijitokeza katika shule hapa nchini. Suala hili nasema si la kufumbia macho na wale wale wote watakaobainika kuhusika na vitendo hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa,” amesema Waziri Ndalichako.

Waziri Ndalichako amewaeleza wanafunzi hao kuwa suala la kupata ushindi ni rahisi lakini kudumu katika ushindi si kazi nyepesi.
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo akizungumza na wajumbe walioshiriki kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Elimu (hawapo pichani) amesisitiza kuwa lengo la utoaji wa tuzo katika Wiki ya Elimu ni kutoa motisha na kuongeza ari kwa wanafunzi ili wafanye bidii katika masomo yao. Hafla ya utoaji wa tuzo hizo umefanyika leo Mkoani Dodoma katika Shule ya Sekondari Dodoma. 

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dk. Binilith Mahenge amewapongeza wanafunzi waliofanya vizuri katika masomo yao kitaifa ambapo amesema Silaha pekee ya ujenzi wa Taifa na rasilimali za Taifa ni Elimu, ambapo pia amewataka wanafunzi kudumisha nidhamu  na maadili.

Akizungumza kwa niaba ya Serikali ya Uingereza katika maadhimisho hayo ya wiki ya Elimu Gertrude Mapunda  amesema serikali ya Uingereza itaendelea kuisaidia  Serikali ya Tanzania katika kuboresha sekta ya Elimu.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akipokea maelezo ya awali kutoka kwa Mkurugenzi wa Sera na Mipango Gerald Mweli kuhusu vigezo vilivyozingatiwa katika kupata wanafunzi bora waliofanya vizuri kitaifa katika masomo yao ya kuhitimu darasa la saba, kidato cha nne na kidato cha sita kwa Shule za serikali na zisizokuwa za Serikali.  

Jumatano, 6 Juni 2018

WAZIRI NDALICHAKO ASHIRIKI KUAGA NA KUZIKA MAPACHA WALIOUNGANA MARIA NA CONSOLATA


·         AWATAKA WATANZANIA KUISHI KWA KUPENDANA
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia amewataka watanzania kujenga tabia ya kupendana, kuvumilia na kuhurumiana katika maisha ya kila siku.

Waziri Ndalichako ameyasema hayo leo mkoani Iringa mara baada ya kuongoza mamia ya wananchi wakati wa ibada ya kuaga miili ya mapacha walioungana Maria na Cosolata katika viwanja vya Chuo Kikuu Cha RUAHA mkoani Iringa.   

Amesema Maria na Consolata katika uhai wao waliishi wakiwa wameungana kwa hiyo waliishi kwa kuvumiliana na kupendana pia.
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akiaga miili ya mapacha walioungana Maria na Consolata katika viwanja vya Chuo Kikuu cha RUAHA Mkoani Iringa.

Amesema, Watanzania wanatakiwa kujiuliza kwa nini Maria na Consolata wamezaliwa Tanzania na Siyo nchi nyingine? amesisitiza kuwa watoto hao wamezaliwa nchini hapa ili iwe funzo kwa watanzania.

Maria na Consolata watazikwa kwenye jeneza moja litakalokuwa na misalaba miwili.
Maria na Consolata Mwakikuti walifariki jumamosi saa mbili usiku Juni 2 mwaka huu na miili yao itapumzishwa kwenye nyumba yao ya milele kwenye makaburi ya viongozi wa Kanisa Katoliki Tosamaganga mkoani Iringa.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako akilia kwa huzuni mara baada ya kuaga miili ya mapacha walioungana Maria na Consolata katika Viwanja vya Chuo Kikuu cha RUAHA Nkoani Iringa.

Kwa upande wake sista Calista Ludega ambaye ni Mkuu wa Shirika la Mtakatifu Theresa wa Mtoto wa Yesu Jimbo Katoliki la Iringa amesema kuwa wamewazika Maria na Consolata mahala wanapolala Masista wa Maria Consolata kwa ajili ya kuwaenzi masista wa Wamishionari wa Consolata kwa kuwa wao wamekuwa sehemu kubwa ya malezi tangu waliopozaliwa watoto hao hadi wanapomaliza maisha yao duniani.

Familia ya Baba na mama wa mapacha hao kutoka Mkoani Mbeya na Kagera, masista wa Consolata wa Iringa na waombolezaji wengine wameungana katika kuwasindikiza katika safari yao ya mwisho duniani.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akiweka saini kitabu cha maombolezo ya Msiba wa mapacha walioungana Maria na Consolata.

OLE NASHA: SERIKALI YAAHIDI KUSHIRIKIANA NA DFID


Serikali imehaidi kuendelea kushirikiana na wadau wa Sekta ya Elimu katika kuhakikisha watoto wa kitanzania wanapata Elimu iliyo bora ili kufikia malengo ya mkakati wa kuwa na uchumi wa viwanda.

 Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mheshimiwa Wiliam Ole Nasha jijini Dar es Salaam katika kikao cha pamoja kilichowakutanisha Wadau wa Elimu walio chini ya Shirika la  Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza-DFID

Naibu Waziri Ole Nasha amesema ushirikiano wa serikali ambao umekuwepo kwa muda mrefu na wadau hao wa Elimu umechangia katika kuhakikisha mtoto wa Kitanzania anapata Elimu iliyo bora.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Wiliam Ole Nasha akizungumza na wajumbe katika kikao kilichoandaliwa na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza-DFID. Kikao hicho kimewashirikisha wadau wa Elimu kutoka EQUIP –T, EP4R, HDIF,GPE, British Council, GPE, na RISE
“Elimu bora kwa kila mtoto wa kitanzania ndiyo msimamo wa Serikali, katika kutekeleza hilo sera ya Elimu bila malipo imekuwa  na baadhi ya chagamoto  na katika kukabiliana nazo ndiyo maana wamekuwepo wadau wa Elimu ambapo sasa wanafanya kazi kwa kushirikiana na Serikali ili kutimiza malengo yanayokusudiwa, kwani hatuwezi kuboresha Elimu kama kila mtu atafanya kazi peke yake, Umoja ni Nguvu.”amesema Mheshimiwa Ole Nasha.

Ole Nasha amesema mpaka sasa wadau hao wa Elimu kupitia Mpango wa Lipa Kulingana na Matokeo (EP4R) wameshatoa  kiasi cha zaidi ya bilioni 200 ambazo zimekusudiwa kufanya uboreshaji wa Miundombinu ya shule za msingi na Sekondari, pamoja na kukarabati na kujenga vyuo vya Ualimu.


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Wiliam Ole Nasha akishiriki katika moja ya majadiliano ya pamoja katika kikao kilichoandaliwa na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza-DFID kikao ambacho kimefanyika jijini Dar es salaam.

Naye Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza-DFID Jane Miller ameishukuru serikali ya Tanzania kwa ushirikiano ambao wamekuwa wakiupata katika kuhakikisha fedha zinazotolewa zinatumika kama zilivyokusdiwa. Kikao hicho kimewashirikisha wadau wa Elimu kutoka EQUIP –T, EP4R,HDIF,GPE, British Council, GPE, na RISE

Jumanne, 29 Mei 2018

PROFESA MDOE ASHIRIKI KONGAMANO LA SAYANSI NA TEKNOLOJIA NCHINI ISRAEL


Naibu Katibu Mkuu Profesa James Mdoe yuko mjini Jerusalem nchini Israel, kwa ajili ya kushiriki kongamano la Mawaziri la kuadhimisha miaka 70 ya Sayansi na Teknolojia katika kuhudumia wanadamu.

Mkutano huo ulioanza jana ulifungukiwa rasmi na Waziri Mkuu wa Israel ambapo Mada kuu ya mkutano huo ni “kufikiria nje ya boksi”.
Naibu Katibu Mkuu Profesa James Mdoe akiwa katika picha ya pamoja na Waziri Mkuu wa Israel wakati wa kuadhimisha miaka 70 ya Sayansi na Teknolojia.

Kongamano hilo la siku 4 linawashirikisha Mawaziri, Naibu Mawaziri na viongozi mbalimbali.
Naibu Katibu Mkuu Profesa James Mdoe akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wengine wa kongamano la Mawaziri la kuadhimisha miaka 70 ya Sayansi na Teknolojia katika kuhudumia wanadamu nchini Israel.

Jumatatu, 28 Mei 2018


To all Heads of Secondary Schools,

RE:  GUIDELINE FOR EAST AFRICAN ESSAY WRITING COMPETITION FOR SECONDARY SCHOOLS 2018

The East African Community Secretariat (EAC) has organized the EAC students essay writing competition for the year 2018.  The Essay writing competition is intended to broaden knowledge of the school going population on EAC activities.  The competition is open to students from Form I to Form IV who are required to write essays between 1000 – 1500 words.  The students are required to begin researching on the topic prior to writing and submitting to their Heads of Schools by 30th July, 2018. 

The topic for the year 2018 in English is:
How can Science and Technology be used to improve the lives of the citizens of the East African Community?”

In Kiswahili
Ni kwa namna gani Sayansi na Teknolojia inaweza kutumika kuimarisha maisha ya wananchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki?”

In French
"Comment pouvons-nous utiliser la Science et la Technologie pour ameliorer la vie des Peuples de la Communauté Est Africaine?”

The Heads of Schools will then be expected to constitute a marking panel which will choose best essays of the school.  The panel should go through the essays (Please do not mark the essays) and choose three essay to be submitted to Permanent Secretary Ministry of Education, Science and Technology by 15th August, 2018.

The following are the guidelines for essay competition:
·  The length of the essay should be between 1,000 and 1,500 words,
·  The essay can be written in English, French or Kiswahili,
·  The essay should be in their own hand writing,
·  Students information such as name, sex, class, school address, region, Country and title of the essay should be written on the cover page,
·  The essay should be written on white A4 lined/ruled papers (Similar to the draft pads),
·  Written only on one side of the paper,
·  Students should draw double margin in each paper,
·  The Head of Schools to certify that the essay is student’s own work. (signature and stamp),
·                 Students to show the reference materials they have used in writing the essay.



Moshi J. Kabengwe
ACTING PERMANENT SECRETARY



Jumapili, 27 Mei 2018

ZAIDI YA BILIONI NNE KUTUMIKA KWENYE MIRADI YA UTAFITI.


·         WAZIRI NDALICHAKO ASISITIZA KUWA ZISITUMIKE VINGINEVYO

Serikali imetoa zaidi ya bilioni nne kwa ajili ya Taasisi na Watafiti walioshinda maandiko ya miradi 8 ya utafiti ambayo itaanza kufadhiliwa mwaka huu wa fedha.

Akizungumza jijini Dar es Salaam kabla ya kukabidhi hundi kwa Taasisi zilizoshinda fedha hizo Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa. Joyce Ndalichako amesema miradi yote iliyopata fedha ni ile ambayo ina malengo madhubuti ya kuimarisha uchumi wa viwanda hadi ifikapo 2025.

Waziri Ndalichako amesema kufadhiliwa kwa miradi hiyo nane kutaleta mchango mkubwa wa uzalishaji wa dawa nchini na kupunguza uagizwaji wa dawa kutoka nje, uboreshaji wa maabara za uhandishi jeni, kuongeza ushindani wa bidhaa, kuongeza uzalishaji wa mazao, uzalishaji wa mimea, pamoja na kuchangia katika uanzishwaji wa viwanda.
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akikabidhi hundi kwa Taasisi na Watafiti walioshinda maandiko ya Miradi ya utafiti unaosimamiwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH)

Waziri Ndalichako amezitaka taasisi zilizopata fedha hizo kuzitumia kwa uadilifu na kwa malengo yaliyokusudiwa na siyo vinginevyo.

Miradi hiyo nane ni pamoja na ule wa umaliziaji wa kiwanda cha uzalishaji wa dawa na maabara ya utafiti ya mabibo, uimarishaji wa miundombinu ya utafiti na ugunduzi wa dawa katika chuo kikuu cha tiba (MUHAS), Muhimbili, ununuzi wa vifaa na uboreshaji wa maabara ya uhandisi jeni ya Taasisi ya Mifugo TALIRI kwa ajili ya kuongeza kasi ya uzalishaji wa mifugo, Uboreshaji wa maabara ya Chanjo ya Taasisi ya Taifa Kibaha.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akipokelewa na baadhi ya watumishi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) mara baada ya kuwasili katika Taasisi hiyo jijini Dar Es Salaam. 

Miradi mingine ni Uboreshaji wa maabara ya udongo, ili kuimarisha Afya ya Udongo kwa ajili ya kilimo endelevu kwa lengo la kuimarisha uchumi wa viwanda, Uboreshaji wa maabara ya kisasa ya utafiti wa mbogamboga na matunda kaskazini mwa Tanzania (HORTI Tengeru), Ukarabati wa mtambo wa utafiti wa kutengeneza mvinyo  katika taasisi ya utafiti wa kilimo, Makutopora na uboreshaji wa usimamizi wa maabara za uchakataji wa mazao ya taasisi ya utafiti wa viwanda TIRDO. 
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH Dk. Amosi Nungu akizungumza na washiriki wa Mkutano wa utoaji wa hundi kwa washindi wa maandiko ya miradi