Jumatano, 3 Julai 2019

WATAALAMU WA SAYANSI WATAKIWA KUSHAURI MATUMIZI YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA KATIKA MAENDELEO


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amewataka wanasayansi wanachama wa Akademia ya Sayansi Tanzania (TAAS), kutumia ujuzi wao kutoa ushauri wa matumizi ya Sayansi na Teknolojia katika shughuli za maendeleo nchini.

Waziri Ndalichako ametoa agizo hilo jijini Dar es Salaam katika hafla ya uzinduzi wa Baraza la tatu la Akademia hiyo ambapo amewataka kuhakikisha wanasimamia vyema ustawi wa Baraza hilo ili liweze kushiriki kikamilifu katika kuhakikisha Sayansi, Teknolojia na Ubunifu vinatumika kama nyenzo ya kuleta maendeleo endelevu ya uchumi nchini.

“Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2016/17 – 2020/21 unalenga kujenga uchumi wa viwanda ili kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025; Mpango umeeleza bayana kuwa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu ni nyezo muhimu katika azma hivyo serikali na wataalamu kama ninyi tuna wajibu wa kuhamasisha matumizi ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu katika jamii,” alisema Waziri Ndalichako.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Baraza la tatu la Akademia ya Sayansi Tanzania Jijini Dar es Salaam.
Alisema ni vizuri Baraza hilo likajikita katika kukuza na kuendeleza Ubunifu na Ugunduzi wa maarifa ya kisayansi katika nyanja za kijamii na kiuchumi kwa kutoa ushauri na maoni kuhusu Sera na mikakati ya kuendeleza Sayansi, Teknolojia na Ubunifu ikiwa ni pamoja na kufanya tafiti za kisayansi zenye kutoa utatuzi wa changamoto katika jamii hasa kipindi hiki dunia inapoelekea katika mapinduzi ya nne ya viwanda.

Kiongozi huyo aliongeza kuwa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imechukua hatua mbalimbali za kuhamasisha matumizi ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu ikiwa ni pamoja na kuboresha miundombinu ya kufundishia katika ngazi zote za elimu ikiwa ni pamoja na kuzindua Mwongozo wa kutambua na kuendeleza Ugunduzi, Ubunifu na Maarifa, kuanzisha vituo vya kulea ubunifu na ugunduzi na kwamba itaendelea kushirikiana na Baraza hilo ili kuhakikisha masuala ya sayansi, teknolojia na ubunifu yanafanikiwa.
Rais mteule wa Baraza Jipya la Akademia ya Sayansi Tanzania, Prof. Yunus Mgaya akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza hilo uliofanyika Jijini Dar es Salaam.
“Utaona katika mwaka wa fedha 2018/2019 Serikali imewawezesha wabunifu 30 kwa kutoa zaidi ya Shilingi bilioni 1, hii inatokana na ukweli kwamba inawatambua na ina lengo la kuendeleza kazi zao,” aliongeza Waziri Ndalichako.

Katika hatua nyingine Waziri Ndalichako amempongeza Rais Mteule wa Baraza jipya la Akademia ya Sayansi Tanzania Prof. Yunus mgaya pamoja na mabaraza yaliyotangulia kwa kuendeleza Akademia hiyo iliyoanza rasmi mwaka 2005, kwani wanachama wake wamekuwa wakifanya kazi mbalimbali za kujitolea na kwamba anatambua mchango wao katika kukuza na kuendeleza matumizi ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu kwa ajili ya maendeleo ya taifa.
Wajumbe wa Baraza la Akademia ya Sayansi Tanzania wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako wakati wa   uzinduzi wa baraza hilo uliofanyika Jijini Dar es Salaam.
Awali akizungumza katika hafla hiyo Rais huyo mteule wa TAAS Mgaya amesema Akademia hiyo imejipanga kuongeza wanachama na kufanya tafiti, kusaidia wanasayansi kuchapisha tafiti hizo katoka majarida yanayotambulika kimataifa, lakini kubwa zaidi ni kuhuisha matumizi ya Sayansi na teknolojia katika maendeleo ya uchumi.

Baraza la Akademia ya Sayansi Tanzania lina wanachama wanasayansi 131 kutoka nyanja mbalimbali za Sayansi nchini.
Mmoja wa wajumbe la Baraza jipya la Akademia ya Sayansi Tanzania, Prof. Julie Makani akipokea vitendea kazi kutoka kwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako.

Rais wa Baraza la Akademia ya Sayansi Tanzania aliyemaliza muda wake, Prof. Esther Mwaikambo akiongea wakati wa hafla ya uzinduzi wa Baraza jipya uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Mtendaji Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) Dkt. Amos Nungu akiongea wakati wa hafla ya uzinduzi wa Baraza jipya uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza la tatu la Akademia ya Sayansi Tanzania mara baada ya uzinduzi wa Baraza hilo.

Jumanne, 2 Julai 2019

NDALICHAKO ATAKA SKAUTI ITUMIKE KUJENGA UZALENDO KWA VIJANA NCHINI


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako, ameuagiza uongozi wa Skauti nchini kuhahakikisha, wanatumia vijana wa skauti kuelimisha na kujenga uzalendo miongoni mwa makundi ya Vijana nchini .

Amesema hayo, katika uzinduzi wa semina elekezi ya Makamishna wa Skauti wa mikoa, Wilaya, Wajumbe wa Bodi na Kamati Tendaji za Skauti Nchini iliyofanyika katika ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza na Skauti wakati wa uzinduzi wa semina elekezi ya Makamishna wa Skauti wa mikoa, Wilaya,  Wajumbe wa Bodi na Kamati Tendaji za Skauti Nchini iliyofanyika katika ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es Salaam.
Ndalichako amepongeza Chama cha Skauti Tanzania pamoja na Zanzibar kwa kushiriki na kufanikisha sherehe za maadhimisho ya Miaka 107 ya Skauti Zanzibar na kwa kuandaa semina hiyo elekezi, ili kuwangejea uwezo viongozi wake hususan katika mambo muhimu katika taifa ambayo kwa kiasi kikubwa yanahitajika kutolewa elimu juu yake kwa vijana ambao ndio nguvu kazi ya Taifa.


Aidha amewataka viongozi hao kutumia Semina hiyo kama nyenzo muhimu itakayowasaidia kuelewa misingi, miongozo, sera na mikakati mbalimbali ili kuwalea vijana wanaowaongoza katika maadii mema ya chama cha Skauti na kupata ujuzi wa kitaalam utakaowawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Waziri Ndalichako ambae pia ni rais wa Skauti Nchini, amesema Wizara ya Elimu kwa kutambua umuhimu wa Skauti Nchini katika malezi ya Vijana imetoa waraka wa kuhuisha uskauti shuleni na vyuoni hivyo kuagiza viongozi katika asasi na taasisi hizo kuhakikisha ustawi wa shughuli za uskauti unaendelea kwa kasi zaidi, huku akiwataka Maafisa Elimu wa Mikoa na Wilaya kuratibu shughuli za Skauti katika maeneo yao, ikiwemo kuhakikisha kuwa walimu wanaosimamia shughuli za Skauti wanapatiwa mafunzo yatakayowawezesha kusimamia vema shughuli hizo.

Waziri Ndalichako amepongeza hatua ya kushirikisha Vyombo vya Serikali kutoa elimu kuhusu masuala muhimu ya mtambuka kwa Taifa, ikiwa ni pamoja na masuala ya mapambano dhidi ya Rushwa na Madawa ya kulevya. Aidha ametumia nafasi hiyo kushukuru vyombo vilivyoshiriki kutoa elimu ikiwemo TAKUKURU, Jeshi la Zimamoto na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na  Dawa za Kulevya.
“Natoa wito kwa washiriki wote kusikiliza kwa makini mada hizo muhimu ili mkazitumie katika kutekeleza jukumu la kuwajengea vijana uzalendo, uadilifu na kuwa mstari wa mbele katika kufanya kazi na kupambana na majanga yanayolikabili Taifa letu.”
Skauti Mkuu Chama Cha Skauti Tanzania Mheshimiwa Mwantumu Mahiza akimkaribisha Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako wakati wa uzinduzi wa semina elekezi ya Makamishna wa Skauti wa mikoa, Wilaya,  Wajumbe wa Bodi na Kamati Tendaji za Skauti Nchini iliyofanyika katika ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es Salaam.
Katika hatua nyingine Ndalichako kwa nafasi yake kama Rais wa chama cha Skauti na Waziri mwenye dhamana ya Elimu, amewaagiza wa Wakuu wa Shule na Wakuu wa Taasisi nyingine zenye vyama vya skauti kusimamia kwa makini shughuli za uskauti na kuepuka matumizi mabaya ya Skauti, ikiwemo kuwapa jukumu la utoaji wa adhabu kwa vijana wenzao.

“ Niombe sana uongozi suala la kutumia vibaya skauti kwa ajili ya kuumiza vijana wenzao lisijirudie tena  kwani lengo la Skauti ni upendo, jambo hili halikunifurhisha, Viongozi simamieni na fundisheni , upendo, amani , umoja na mshikamano ambazo ni nguzo kuu za taifa letu, kwa jinsi hii tukuwa na vijana shupavu wazalendo wachapakazi,ambapo tutakuwa tunaunga mkono kwa vitendo juhudi za Rais wetu Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ambae anasisitiza juu ya amani na uchapakazi katika kuifikisha nchi yetu katika uchumi wa kati ifikapo 2025 kupitia viwanda.”

Akizungumza kabla ya kumkaribisha waziri Ndalichako  Skauti Mkuu - Chama Cha Skauti Tanzania Mheshimiwa Mwantumu Mahiza, alimshukuru Waziri kwa kukubali mualiko na kusema kuwa Chama hicho kinaendelea kufanya kazi zake kimkakati  ikiwemo kutekeleza jukumu lake kubwa la kulea vijana, kuwajenga kuwa wazalendo walio tayari kulitumikia taifa.

Nae mlezi mteule wa Chama hicho Askofu Gervas John Mwasikwabhila Nyaisonga, Askofu Mkuu Jimbo la Mbeya Kanisa katoliki na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC),lakini pia ni Skauti, ameishukuru Serikali kwa uteuzi wake akiwa mlezi wa tatu  katika Chama hicho. Walezi wengine, ni Rais Msataafu Mheshimiwa Ali Hassan Mwinyi na Mheshimiwa Balozi Salim Ahmed Salim.  Aidha Askofu Nyaisonga ameahidi kuwa Skauti itayafanyia kazi maagizo ya Waziri kwa wakati na kuendelea kutoa kuduma bora kwa weledi popote watakapo hitajika.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akikagua gwaride la Skauti lililoandaliwa kwa ajili yake wakati wa wakati wa uzinduzi wa semina elekezi ya Makamishna wa Skauti wa mikoa, Wilaya,  Wajumbe wa Bodi na Kamati Tendaji za Skauti.

Jumatatu, 1 Julai 2019

TANGAZO


UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY




STUDY OPPORTUNITY TENABLE AT REGIONAL SCHOLARSHIP AND INNOVATION FUND HOST UNIVERSITIES (RSIF-AHU)  2019/2020

Call for Application
The General Public is hereby informed that, the  Regional Scholarship and Innovation Fund (RSIF) which is the flagship Partnership for Skills in Applied Sciences, Engineering and Technology (PASET-RSIF) Programme offers  Scholarship opportunities  to Tanzanians to study  various PhD programmes in the RSIF African Host Universities such as Sokoine Uniersity of Agriculture (SUA) and  The Nelson Mandela African Institution of Science and Technology (NM-AIST) in Tanzania, University of Gaston Berger (UGB) in Senegal, University Félix Houphouët-Boigny (U-FHB) in Ivory Coast, Kenyatta University (KU) and University of Nairobi (UON) in Kenya, University of Port Harcourt, African University of Science and Technology (AUST) and Bayero University Kano (BUK) in Nigeria, University of Ghana (UG), Ghana, University of Rwanda (UR) in Rwanda. The scholarship focuses on the following programme priority areas.

     1.      ICTs, including big data and artificial intelligence;
     2.      Food security and agribusiness;
     3.      Minerals, mining and materials engineering;
     4.      Energy including renewables; and
     5.      Climate change.

Eligibility criteria
To be eligible for this scholarship, applicants should meet the following criteria:
1.      Master’s degree in  relevant field of study;
2.   The Citizens of  United Republic of Tanzania willing to enroll full-time in a PhD program at an RSIF African Host University; and
3.    Demonstrate leadership potential, such as community service in areas related to PASET RSIF fields of study.
4.   NB: Priority will be given to women and existing young academic staff at African Universities

Application Procedure 
Completed application forms and accompanying supporting documents must be submitted online through the following website https://app.rsif-paset.org/rsif-applications-2019/index.php
Further information on the PhD program specific requirements and  RSIF African Host Universities  (RSIF AHU) admissions criteria can be found here: https://www.rsif-paset.org/calls/2019-call-applications/

Submission:
Deadline for online applications: 22nd  July 2019 at 5:00pm (GMT).

Issued by:
Permanent Secretary,
Ministry of Education, Science and Technology,
University of Dodoma,
College of Business and Law,
Block 10,
P. O. Box 10,
40479 DODOMA.