Ijumaa, 26 Julai 2019

TAARIFA KWA UMMA


UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY

SCHOLARSHIPS TENABLE IN THE PEOPLE’S DEMOCRATIC REPUBLIC OF ALGERIA FOR ACADEMIC YEAR 2019/2020

Call for Applications
The General Public is hereby informed that, the People’s Democratic Republic of Algeria  has granted a Scholarship programme to eligible Tanzanian Nationals to pursue Undergraduate studies at Universities in Algeria for the academic year 2019/2020 in the following field categories:

Category A. Higher Education
      1.      Medicine;
      2.      Technical Sciences;
      3.      Science of Matter;
      4.      Mathematics and Computer;
      5.      French;
      6.      Science of Nature and Life; and
      7.      Earth Science and the Universe.

Category B. Religious Affairs and Academic
1.         Imam preacher and/or Quran teacher;
2.         Bachelor degree (Licence) in Imamat.

Application Requirements
1.      Must have completed Advanced Secondary School or Diploma in 2017-2018;
2.      Will be not more than 25 years of age by October, 2019;
3.      Medical Examination Certificate from a Public Hospital; 
4.  Have a good knowledge of the Holy Quran for Imam Preacher/or Koran teacher applicants;
           5.    Have a good knowledge of the Holy Quran for Bachelor degree in Imamat 
            applicants.

Application Package
  §      Certified copies of;
-         Certificate of Secondary Education Examination (CSEE);
-         Certificate of Advanced Secondary Education Examination (ACSEE) or Diploma Certificates (Academic Certificates and Transcripts);
-         Birth Certificates;
  §      Application letter (with your contacts; telephone number and email address); and
     §    Medical Examination Certified by a Public Hospital;

NB:
     ·        Selected applicants will undergo one year for French language before commencing undergraduate degree studies.
     ·        There is no Loan or grant  from the Government of Tanzania  for candidates who will be offered this Scholarship.

Mode of Application
All applicants should submit their application packages to reach the undersigned  not later than 1630Hrs on 10th August 2019 to:

Permanent Secretary,
Ministry of Education, Science and Technology,
University of Dodoma (UDOM)
Business School,
Block 10,
40479 DODOMA.

Jumamosi, 20 Julai 2019

WAZIRI NDALICHAKO ATAKA USIMAMIZI THABITI UDAHILI WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako ametoa wito kwa Viongozi wa Elimu ya juu nchini kuhakikisha wanasimamia ipasavyo mchakato wa udahili wa wanafunzi wa elimu ya juu kwa mwaka wa masomo 2019/20 ili kuondoa usumbufu usiokuwa wa lazima kwa wanafunzi, wazazi, walezi na wafadhili wa wanafunzi hao.

Waziri Ndalichako ametoa wito huo Jijini Dar es Salaam wakati akifunga maonesho ya 14 ya elimu ya juu yaliyofanyika katika viwanja vya Mnazi ambayo yalikuwa na kauli mbiu isemayo Jukumu la Taasisi za Elimu ya Juu Katika Kuzalisha Ujuzi Unaohitajika kwa ajili ya Viwanda.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akipata maelezo ya programu zinazotolewa na Chuo Kikuu Dodoma wakati wa maonesho ya 14 ya elimu ya Juu yalivyofanyika katika viwanja vya Mnazi mmoja Jijini Dar es Salaam.
Katika hotuba yake amesema asingependa kuona changamoto zilizotokea mwaka jana katika kujiunga na vyuo zinajirudia kwani changamoto nyingine zilisababishwa na Vyuo vyenyewe kutokuwa na mifumo thabiti ambayo wanafunzi wangeweza kufanya maombi na kujithibitisha katika vyuo kwa urahisi.

“Nafahamu kwamba TCU wameshatoa mafunzo na maelekezo ya kutosha kwa wataalamu wa mifumo ya kompyuta na maafisa udahili wa vyuo vyote ambao mnadahili wanafunzi kwa mwaka wa masomo 2019/20 kwa hiyo naamini kwamba zoezi la udahili kwa mwaka huu litafanyika kwa ufanisi zaidi kuliko ilivyokuwa mwaka jana,” alisema Waziri Ndalichako.

Waziri Ndalichako  alisistiza kuwa kwa mujibu wa sheria ya vyuo vikuu sura ya 346 ya sheria za Tanzania jukumu la kudahili wanafunzi ni la Seneti za Vyuo Vikuu au Bodi ya za Chuo husika, hivyo amewataka Viongozi wa Vyuo kutumia mamlaka ya Seneti za Vyuo Vikuu au Bodi kuhakikisha kuwa wanasimamia kikamilifu udahili wa wanafunzi ili waweze kujiunga kwa urahisi huku akisistiza pia  vigezo, masharti, taratibu na sifa za mwanafunzi kujiunga na chuo kuzingatiwa.

“Niwakumbushe tu  Serikali iko macho, katika mchakato wa udahili msipofuata taratibu mkaweka watu wasio kuwa na sifa tutawaondoa lakini kumbukeni na ninyi mloiwaingiza hamtabaki salama, hakikisheni zoezi hilo linafanyika kwa ufanisi,”aliongeza Waziri Ndalichako.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akipata maelezo katika banda la DIT wakati wa maonesho ya 14 ya elimu ya Juu yaliyofanyika katika viwanja vya Mnazi mmoja Jijini Dar es Salaam


Sambamba na hilo amewataka wanafunzi wanaotarajia kujiunga na masomo ya elimu ya juu kutokuwa wavivu wa kusoma maelekezo kabla ya kuanza kujiunga ama  kuchagua kozi katika vyuo. Amewaasa kuzingatia sifa zinazohitajika kwa kulinganisha ufaulu wao wakati wa kuchagua kozi huku akisistiza kuwa Serikali haina utaratibu wa kumpangia mwanafunzi programu ya kusoma isipokuwa inachagua mwanafunzi kutokana na sifa alizonazo katika kozi husika.

Katika hatua nyingine Waziri Ndalichako amezitaka Taasisi za Elimu ya juu na Vyuo vikuu kuendelea kujitathmini ni kwa kiasi gani  tafiti ambazo wamekuwa wakizifanya zinagusa moja kwa moja jamii na kusaidia kutatua changamoto mbalimbali  zilizopo katika jamii.

“Ninyi Taasisi za Elimu ya Juu macho yenu na masikio yawe wazi kila mara ili muweze kusikiliza wapi katiika jamii kuna changamoto na kwa kutumia utaalamu wenu mshiriki kuzitatua, kumbukeni elimu ya juu katika nchi yoyote ile ndio kitovu cha maarifa hivyo muendelee kutumika katika kutatua changamoto hizo,” aliongeza waziri Ndalichako.

 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza na baadhi ya wanafunzi waliofika katika viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam kutembelea maonesho ya 14 ya elimu ya juu.

Akizungumza kwa niaba ya washiriki wa maonesho Profesa Uswegi Minga Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Tumaini amesema uwepo wa maonesho hayo umetoa nafasi ya vyuo vyenyewe kujitangaza kuhusu fursa zinazopatikana katika vyuo vyao, lakini pia imekuwa nafasi nzuri ya kubadilishana uzoefu  kutokana na kujifunza namna vyuo vingine vinavyofanya kazi hivyo kusaidia kufanya maboresho katika maeneo ya uendeshaji wa Vyuo lakini pia katika upangaji na ufundishaji wa programu mbalimbali.

Maonesho ya 14 ya Vyuo vya Elimu ya Juu yameandaliwa na Tume ya Vyuo Vikuu nchini na kwa mwaka huu yamekuwa na washiri zaidi ya 80 vikiwemo kutoka nje ya nchi na vile vyaTanzania.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akigawa cheti kwa moja ya Taasisi ambayo imeshiriki katika maonesho ya 14 ya elimu ya ju. Maonesho hayo yamefanyika  katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Da res Salaam.

Ijumaa, 19 Julai 2019

TCU KUHAKIKISHA MITAALA KATIKA VYUO VIKUU INAANDAA WAHITIMU WANAOENDANA NA MATAKWA YA TAIFA

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassimu Majaliwa (Mb) ameitaka Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) nchini kuhakikisha mitaala inayotumika katika vyuo vikuu iweze kuandaa wahitimu siyo tu kwa kuajiriwa, bali pia kuwa na uwezo wa kujiajiri na kutengeneza ajira kwa wengine.

Waziri Mkuu Majaliwa ametoa agizo hilo jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa maonesho ya 14 ya elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia nchini ambapo amesema uwepo wa mitaala ya aina hiyo utasaidia kuchochea kasi ya ukuaji wa uchumi na maendeleo ya watu kwa ujumla.

“Nimeelezwa kuwa tayari baadhi ya Vyuo Vikuu na Taasisi za Elimu ya Juu zimeshaanza kuchukua hatua za kutengeneza Mitaala mipya na kuhuisha ile ya zamani ili kuifanya iendane na mahitaji ya sasa ya taifa na soko la ajira, nitoe wito kwa Taasisi zote za Elimu ya Juu kuendelea kuhuisha na kuboresha mitaala yao kwa mwelekeo huo,” alisema Mhe Majaliwa.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha akisalimiana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (MB) wakati alipowasili viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam ili kufungua maoesho ya 14 ya Elimu ya Juu Tanzania. 
Akizungumzia azma ya serikali ya kuongeza udahili katika Vyuo Vikuu, Waziri Mkuu ameitaka Tume ya Vikuu kutafuta mbinu za kuviwezesha vyuo zaidi ikiwa ni pamoja na kujengea uwezo vyuo vikuu binafsi ili visaidie katika kuongeza udahili pamoja na kufikia viwango vinavyotakiwa na siyo kuwapunguzia viwango vya matakwa ya usajili.

“Msimamo wa Serikali uko wazi na unataka Vyuo Vikuu Binafsi kuwa washirika muhimu kwenye maendeleo ya Sekta ya Elimu ya Juu nchini, hata hivyo nai vema nikaeleweka vizuri hakuna mbadala wa elimu bora, ni wajibu wetu  kuhahakikisha vyuo vyote vinatoa elimu bora. TCU endeleeni kutekeleza majukumu yenu  ya kimsingi ya kudhibiti na kushauri lakini zaidi jipambanue  katika uwezeshaji wa vyuo hivyo ili kuondoa taswira hasi iliyojengeka katika jamii kuwa kazi ya Tume  ni kuvifungia vyuo vikuu badala ya kutatua changamoto zinazowakabili.” Alisema Mhe. Majaliwa.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (MB) akipata maelezo ya kazi zinazotekelezwa na Tume na Vyuo Vikuu nchini (TCU) kutoka kwa Katibu Mtendaji wa Tume hiyo Profesa Charles Kihampa. Taasisi hiyo ndio mratibu wa maoesho ya Taasisi ya Elimu ya Juu yanayofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja  jijini Dar es Salaam.
Alisema ili kuongeza idadi ya watanzania wanaopata nafasi ya Elimu ya Juu, ni lazima kama nchi kupanga mikakati kwa kushirikiana na sekta binafsi, ambao ni wadau wakubwa sana katika Elimu ya Juu kwani ukiangalia kati ya wahitimu wote wa Vyuo vikuu kwa mwaka, asilimia 25 wanatoka katika vyuo vikuu binafsi.

Katika hatua nyingine Mhe. Majaliwa ameitaka TCU kuhakikisha wanakutana na taasisi binafsi zinaowasaidia watanzania kupata nafasi katika vyuo vikuu nje ya nchi ili ziweze kuwatambua, kuwasajili lakini pia kufanya nao kazi kwa karibu ili kuwaambia mahitaji halisi ya kwenda vyuo vikuu ni yapi na wao washiriki katika kumshauri kijana ni alama zipi za ufaulu zinafaa kwenda kwenye digrii, diploma na ama cheti ili kuepukana na changamoto ya kutotambulika kwa vyeti pindi wanapohitimu katika ngazi hizo za elimu akitolea mfano watanzania ambao wamesoma kwenye moja ya Chuo Kikuu kilichopo nchini Misri lakini vyeti vyao kutotambulika.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (MB) akizungumza wakati wa ufunguzi wa maoesho ya 14 ya Elimu ya Juu Tanzania yaliyofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam. 
 “Naona kundi kubwa la vijana wa kidato cha sita wanatafuta vyuo kupitia taasisi hizo ni vyema sasa TCU kwa kuwa mko katika maonesho hayo mshirikiane kuwasaidia vijana wetu hawa kupata vyuo vinavyostahiki ili wakienda kusoma akipata cheti na kurejea muweze kuvitambua vyeti hivyo,” alisema Mhe. Majaliwa

Awali Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William ole Nasha alimweleza Waziri Mkuu kuwa ili kuongeza idadi ya wahitimu watakaochochea ukuaji uchumi kwa kupitia sekta zinazochangia kwa kiasi kikubwa kukua kwa uchumi tayari baadhi ya vyuo vimefanya maboresho ya mitaala kutoka kwenye mfumo unaozingatia ufahamu na kwenda kwenye mfumo wa umahiri.

Pia Wizara kwa kushirikiana na Taasisi za sekta binafsi Tanzania imeanzisha mabaraza 6 ya kisekta ya ujuzi na maarifa katika Sekta za Kilimo, Ujenzi, Uchukuzi, Utalii, Nishati na TEHAMA kwa lengo la kushauri kuhusu mitaala na mahitaji halisi ya soko la ajira.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi waliotembelea banda la Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wakati wa maoesho ya 14 ya Elimu ya Juu Tanzania yanayofanyika Jijini Dar es Salaam.
Nae Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu nchini Charles Kihampa amesema Maonesho ya Vyuo Vikuu kwa mwaka huu yamehudhuriwa na taasisi 81 ambapo taasisi 66 ni za ndani ya nchi na 15 ni taasisi za kutoka nje ya nchi.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa maonesho ya 14 ya elimu ya Juu Mwenyeketi wa Kamati ya Wakuu wa Vyuo vikuu vya Umma nchini Prof. Raphael Chibunda ameipongeza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Serikali kwa Ujumla kwa kuhakikisha kuwa Mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu inaongezeka jambo ambalo limepunguza migogoro katika Vyuo.

Maonesho ya 14 ya Elimu ya Juu yana kauli mbiu isemayo Jukumu la Taasisi za Elimu ya Juu katika kuzalisha Ujuzi unaohitajika kwa ajili ya Viwanda.
Mmoja wa watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia akitoa ufafanuzi kwa wadau waliotembelea banda la Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia katika maonesho ya 14 ya Elimu ya Juu Tanzania yanayofanyika jijini Dar es Salaam.

TAARIFA KWA UMMA


UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY




UNDERGRADUATE SCHOLARSHIPS TENABLE IN ROMANIA DURING ACADEMIC YEAR 2019-2020

Call for Applications
The General Public is hereby informed that, the Government of Romania has granted a Scholarship programme to eligible Tanzanian Nationals to pursue undergraduate studies at Universities in Romania. The Scholarship programme is scheduled to start during 2019/2020 academic year at the following Universities:-

1.    The National University of Political Studies and Public Administration  specializing in the fields of Political Science, Public Administration, Management, Communications and Public Relations, International Relations and European studies. http://snspa.ro/en/study-snspa/admission/non-eu-students/

2. The University of Medicine, Pharmacy, Science and Technology of Târgu Mureș https://www.umfst.ro/admission/admission-2019.html

3.    The University of Agronomic Sciences and Veterinary Medicine of Bucharest specializing in the fields of Agronomic Sciences, Veterinary Medicine, Biotechnologies, Land Reclamation, Horticulture https://www.usamv.ro/index.php/en/admission-2018

4.    Lucian Blaga” University of Sibiu specializing in the fields of  Letters, History and Law, Medicine, Food and Textile Processing Technology, Engineering and Sciences  https://admitere.ulbsibiu.ro/ro/oferta/non-eu-citizens/

5.  Transilvania University of Brasov specializing in the fields of Mechanical Engineering, Technological Engineering, Civil Engineering, Materials Science and Engineering, Electrical Engineering and Computer Science, Food and Tourism, Wood Processing, Forestry, Economics, Mathematics and Computer Science, Music, Medicine, Law, Sociology and Communication, Sports and Physical Education, Letters, Product Design and Environment, Psychology and Education Sciences. https://www.unitbv.ro/en/prospective-students/admission/admission-information-for-non-eu-citizens.html

6.  West University of Timisoara specializing in the fields of Chemistry , Biology and Geography, Economics and Business Administration, Mathematics and Computer Science, Music and Theatre, Political Sciences, Philosophy and Communication Sciences. https://ri.uvt.ro/cetateni-din-state-terte-uniunii-europene-2/?lang=en

7.   Aurel Vlaicu” University of Arad specializing in the fields of Design, Economic Sciences, Exact Sciences, Humanities and Social Sciences, Educational Sciences, Psychology and Social Sciences, Theology, Engineering, Food Engineering, Tourism and Environmental Protection, Physical Education and Sport. https://www.uav.ro/en/admission/how-to-apply/non-eu-citizens

      The application package should comprise of the following:
(i)      Application form for the issuance of the Acceptance Letter, filled in ALL the fields (attached);  https://drive.google.com/open?id=1AvowzhFaxvp82rqJlz03yp6_SXr3T6pb
(ii)            Proof of Nationality;
(iii)          Birth Certificate;
(iv)          A level ACSE Results Transcripts;
(v)            O level CSE Results Transcripts;
(vi)          Diploma Results certificates and Transcripts;
(vii)        Medical Examination Certificate from a  Government Hospital; and
(viii)     A copy of the marriage certificate (if the applicant’s name changed subsequent to the marriage).

Note: In case the above documents are not in English/French/Romanian you should submit a copy of legalized translation.

Application Procedure
Scanned application package should be sent directly to the respective Universities in Romania not later than 20th July 2019.

Jumatano, 10 Julai 2019

BILIONI 40 KUJENGA VYUO VYA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI STADI KATIKA WILAYA 25


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amezindua Chuo cha Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) cha Wilaya ya Urambo ambapo amesema serikali katika bajeti ya mwaka  huu imetenga jumla ya Shilingi bilioni 40  kwa ajili ya kujenga vyuo vipya  katika wilaya 25.

Waziri Ndalichako ametoa kauli hiyo mkoani Tabora wakati wa uzinduzi wa chuo hicho ambapo amesema ongezeko la vyuo vya ufundi nchini linasaidia kuongeza idadi ya wanafunzi wanaopata elimu ya ufundi ambao wanahitajika katika viwanda mbalimbali  vinavyoanzishwa nchini.

"Kadri tunavyoongeza vyuo hivi vya ufundi katika wilaya mbalimbali tunasogeza elimu  ya ufundi itolewayo na vyuo vya VETA karibu na wananchi ili kuwawezesha kupata ujuzi na stadi zinazohitajika katika kipindi hiki ambacho nchi yetu inalenga kujenga uchumi wa viwanda kuiwezesha kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025, " amesema Ndalichako.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza na viongozi  mbalimbali wa Serikali na  wananchi wa Mkoa wa Tabora (Hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa Chuo cha Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA)

Amesema dira iliyowekwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ya kujenga uchumi wa viwanda imekuwa chachu kwa wizara kuongeza kasi ya huduma ya mafunzo ya ufundi stadi ambapo mpaka sasa inakamilisha vyuo vya VETA katika Wilaya za Nkasi, Ileje, Newala na Muleba ambavyo vipo katika hatua za ukamilishaji.  Vyuo vingine vilivyo katika hatua ya ujenzi ni vya halmashauri ya Kasulu, Itilima, Ngorongoro, Chato, na Babati ambavyo vinatarajiwa kukamilika kabla ya kumaliza mwaka huu 2019.










 
Waziri Ndalichako amezitaja wilaya nyingine ambazo zitajengewa vyuo hivyo kuwa ni pamoja na Wilaya za Chunya, Kilindi, Korogwe, Ukerewe, Igunga, Pangani, Kishapu, Rufiji, Uyui, Kwimba, Bahi, Mafia, Longido, Mkinga, Uvinza, Ikungi, Iringa Vijijini, Lushoto, Mbarali, Monduli, Buhigwe, Ulanga, Masasi, Butiama na Chemba.

Aidha, Waziri Ndalichako amewashukuru Viongozi wa Mkoa wa Tabora, Halmashauri ya Wilaya ya Urambo, Mbunge wa Jimbo la Urambo, Mhe. Margreth Sitta na wananchi wote wa Wilaya hiyo kwa utayari wao wa kuhakikisha upatikanaji wa majengo na eneo lenye ukubwa wa mita za mraba 45,000 kwa ajili ya Chuo cha VETA cha Urambo.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako pamoja na Viongozi wengine wakifurahia jambo mara baada ya kuzindua Chuo cha VETA cha wilaya ya Urambo Mkoani Tabora aliyevaa koti ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora


Wakati huo huo Waziri Ndalichako ametumia nafasi hiyo kuagiza Uongozi wa VETA kukamilisha ujenzi unaoendelea wa vyuo vya VETA katika wilaya kwa wakati na ubora

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanry, akizungumza katika uzinduzi huo, amewataka vijana wa wilaya ya Urambo kujiunga na chuo hicho ili kupata ujuzi na stadi zitakazowawezesha kufanya kazi katika miradi ya ujenzi ya kimkakati ya mkoa huo.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako, Mbunge wa Urambo Magreth Sit, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanry pamoja na Viongozi wengine wakikata utepe kuashiria uzindua wa Chuo cha VETA cha wilaya ya Urambo Mkoani Tabora.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa VETA Dkt. Pancras Bujulu, akitoa Maelezo  ya mradi huo amesema umehusisha ukarabati wa majengo, ununuzi wa samani za ofisi, vifaa na vitendea kazi vya ofisi , zana za kufundishia na  samani za mabweni ya wanafunzi umegharimu zaidi ya shlingi milioni 200.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako, akikagua baadhi ya vifaa vya kufundishia na kujifunzia vilivyonunuliwa kwa ajili ya Chuo cha VETA cha wilaya ya Urambo Mkoani Tabora.