Alhamisi, 6 Februari 2020

SERIKALI KUJENGA SHULE ZA WANAFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUM KILA MKOA

Serikali imesema itaendelea na mpango mkakati wa kutekeleza elimu bila malipo pamoja na kutoa vipaumbele kwa watu wenye ulemavu kupata elimu iliyo bora.

Hayo yameelezwa jijini Dar es Salaam na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Ave Maria Semakafu wakati wa ufungaji wa mafunzo ya TEHAMA na Teknolojia Saidizi kwa wakufunzi na walimu wa Sekondari wenye mahitaji maalum.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Ave Maria Semakafu akiongea wakati wa ufungaji wa mafunzo ya Tehama na Teknolojia Saidizi kwa Wakufunzi na Walimu wa Sekondari wenye mahitaji maalumu jijini Dar es Salaam.
Dk. Semakafu amesema  serikali imejipanga kuhakikisha walimu  na wanafunzi wanapata elimu ya Tehama, elimu jumuishi sambamba na kujenga shule zao maalum katika kila mkoa ambapo kwa sasa wameanza na mkoa wa Katavi.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Ave Maria Semakafu akitoa maelekezo kwa mmoja wa washiriki wa mafunzo ya Tehama na Teknolojia Saidizi OUT, jijini Dar es Salaam.
Hata hivyo awali ilielezwa kuwa tayari serikali imetumia kiasi cha shilingi bilioni 5.9 kwa ajili ya kununua na kusambaza vifaa maalum vya kielimu saidizi katika shule za msingi na sekondari zinazopokea wanafunzi wenye mahitaji maalum nchini.

“Hii kazi pia si ndogo, napenda kwa namna ya kipekee kabisa kutumia nafasi hii kuushukuru Uongozi wa Chuo Kikuu Huria kwa kukubali kuendesha mafunzo haya hapa chuoni na kutoa wawezeshaji, vifaa pamoja na miundombinu mingine kwa ajili ya kufanikisha mafunzo haya muhimu,’’ amesema Dk. Semakafu.
Mmoja wa washiriki wa mafunzo ya Tehama na Teknolojia Saidizi akiwa katika mafunzo yaliyofanyika Chuo Kikuu Huria jijini Dar es Salaam.  Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Ave Maria Semakafu.
Aliongeza kuwa mafunzo waliyoyapata ni muhimu kwani yatawasaidia katika matumizi ya TEHAMA kwenye  ufundishaji na ujifunzaji, kutafuta rejea mbalimbali za kielektroniki kwenye mitandao na kutumia teknolojia saidizi zinazowezesha matumizi ya TEHAMA katika ufundishaji na ujifunzaji.

Akizungumza kwa niaba ya washiriki wa mafunzo hayo, Mwalimu wa shule ya sekondari ya Binti Mussa iliyopo Kiwalani jijini Dar es Salaam, Anna Mbogo alisema wanaishukuru kwa  dhati  Wizara ya Elimu kwa kuona umuhimu wa kutoa  mafunzo kwa walimu wenye mahitaji maalum.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya Tehama na Teknolojia Saidizi kwa Wakufunzi na Walimu wa sekondari wenye mahitaji maalumu wakifuatilia hotuba ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Ave Maria Semakafu (hayupo pichani)  wakati wa kufunga mafunzo hayo jijini Dar es Salaam.
“Mafunzo haya  yalilenga kutujengea uwezo sisi walimu kuendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia ya sasa, pia tunaushukuru uongozi wa OUT chini ya serikali ya awamu ya tano kuonesha bayana nia ya kuwasaidia walimu wenye mahitaji maalum na kuwathamini watu wenye ulemavu kwa kuajiri watu wenye ulemavu,’’ amesema Mwalimu Anna.

MAKISATU 2020 KUENDELEA KUIBUA WABUNIFU

Serikali imesema inatambua umuhimu na mchango wa ubunifu na teknolojia katika kurahisisha na kuongeza ufanisi  katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma kuhusu kuanza kwa Mashindano ya Kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU) 2020, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha amesema  mashindano hayo ni moja ya mikakati ya Serikali ya kuibua, kutambua na kuendeleza ubunifu na ugunduzi unaofanywa na watanzania.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Mkutano mara baada ya kuzungumza na Waandishi wa habari jijini Dodoma.  Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Leonard Akwilapo na kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano, Sylvia Lupembe.

"Lengo kubwa la MAKISATU pamoja na kukuza na kusaidia kubiasharisha, yanatoa fursa kwa wabunifu na wagunduzi wa teknolojia mbalimbali kujitangaza na kutangaza kwa wadau ubunifu unaozalishwa," amesisitiza Ole Nasha.
Mwakilishi wa Benki ya CRDB, Prosper Nambaya akizungumza wakati wa Mkutano wa Waandishi wa habari kuzungumzia kuanza kwa mashindano ya MAKISATU, 2020 jijini Dodoma.
Ole Nasha amesema MAKISATU inawalenga wabunifu kutoka makundi ya shule za msingi, sekondari, vyuo vya ufundi stadi, vyuo vya kati, vyuo vikuu, Taasisi za utafiti na Mfumo usio rasmi.

Baadhi ya washiriki waliohudhuria Mkutano wa kuzungumzia kuanza kwa Mashindano ya Kitaifa ya Sayansi, Teknonojia na Ubunifu (MAKISATU) 2020 jijini Dodoma, wakimsikiza Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha (hayupo pichani) wakati akizungumza na Waandishi wa habari.

Aliongeza kuwa kupitia MAKISATU 2019 Serikali imewaibua na kuwatambua wabunifu wachanga zaidi ya 415 huku wabunifu 60 mahiri wakiendelezwa ili ubunifu wao ufikie hatua ya kubiasharishwa.


Kiongozi huyo ametoa wito kwa watanzania wenye ubunifu mbalimbali kushiriki katika mashindani hayo na amewashukuru Benki ya CRDB kwa kukubali kufadhili mashindano hayo.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Wateja Wakubwa kutoka CRDB, Prosper Nambaya amesema Benki hiyo imeamua kuwa na ushirikiano endelevu na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ili kusaidia kukuza ubunifu unaozalishwa nchini kutokana na kuwepo kwa watu wengi wenye mawazo ya kibunifu yanayopaswa kuendelezwa.

Jumatatu, 27 Januari 2020

WALIMU NA WAKUFUNZI 140 WENYE MAHITAJI MAALUM WANAPATA MAFUNZO YA TEHAMA

Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Awamu ya tano imetumiza Sh.bilioni 5.9 kununua na kusambaza vifaa maalum vya kielimu na saidizi katika shule za msingi na sekondari, zinazopokea  wanafunzi wenye mahitaji maalum nchini.

Hayo yamesemwa Jijiji Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo wakati wa ufunguzi wa  mafunzo ya ya siku 10 ya Tehama na Teknolojia saidizi kwa wakufunzi na walimu wenye mahitaji maalumu wanaofundisha shule za sekondari  ili kuwajengea uwezo wa matumizi ya Teknolojia hiyo katika utekelezaji wa majukumu yao.

Kiongozi huyo ametaja vifaa vilivyonunuliwa na kusambazwa kuwa ni Shime sikio (Hearing Aids) kwa ajili ya wanafunzi wenye baki ya usikivu, mashine za kuandikia maandishi ya breli na Vivunge vyenye fimbo nyeupe (Braille kit)kwa ajili ya wasioona.

Alisema  kuwa katika kipindi cha miaka minne ya Rais John Magufuli,  pia Serikali imefanya upanuzi na ukarabati wa Chuo cha Ualimu Patandi ili kuongeza udahili wa walimu kutoka walimu 300 na kufikia walimu 450 kwa mwaka wa masomo 2019/2020.

Pia imejenga  shule ya sekondari ya mfano katika chuo hicho yenye uwezo wa kudahili wanafunzi 640 wenye mahitaji maalum.

Aidha, shule hiyo  itasaidia wanachuo kufanya mazoezi ya kufundisha wanafunzi wenye mahitaji maalumu kwa vitendo na kuwa mahiri katika fani wanazosomea.

“Mnaweza kuona jitihada ambazo serikali imekuwa ikizifanya nitoe wito kwa familia, na wadau wa maendeleo kuendelea kuona umuhimu wa kuchangia juhudi za serikali katika kuwapatia huduma stahihiki wanafunzi wenye mahitaji maalum ili kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika ujifunzaji, " alisema Katibu Mkuu Akwilapo

Dkt. Akwilapo amesema ushiriki wa jamii ni muhimu sana  kwani masuala ya watu wenye ulemavu ni mtambuka hivyo jitihada za pamoja zinahitajika ili kufikia malengo yaliyoanishwa katika miongozo ya kitaifa na kimataifa.

Akizungumzia mafunzo ya TEHAMA na Teknolojia saidizi yanayotolewa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Katibu Mkuu huyo amesema  yanalenga kuwajengea uwezo wakufunzi na walimu wa Sekondari wasioona, viziwi na wenye ualbino  katika matumizi ya TEHAMA na teknolojia saidizi ili  kuboresha ufundishaji katika vyuo vya ualimu na shule za sekondari nchini.

Aliongeza kuwa mafunzo hayo yatawapatia maarifa na stadi kuhusu mfumo, vipengele na utendaji kazi wa kompyuta, utumiaji wa program saidizi za sauti na kukuza maandishi katika kompyuta, kupata stadi za matumizi ya mitandao katika kutafuta na kutuma taarifa mbalimbali katika tovuti na barua pepe pamoja  na kutumia kikamilifu maudhui ya kielektroniki katika ufundishaji na ujifunzaji.

Kwa upande wake Kaimu Kamishna wa Elimu Paulina Mkonongo  alisema, kufanyika kwa mafunzo hayo ni mkakati endelevu wa Serikali kuhakikisha elimu bora inatolewa kwa makundi yote ikiwemo kuimarisha mafunzo kazini kwa kundi hili maalum.

Awali Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu Maalumu Greyson Mlanga ameeleza kuwa mafunzo hayo yana jumla ya washiriki  140 wenye mahitaji maalumu, wakiwemo viziwi 37, wasioona na wenye uoni hafifu 103  kutoka vyuo vya ualimu vya serikali na walimu wa shule za sekondari nchini.

Akizungumza kwa niaba ya washiriki wa mafunzo, Mkufunzi kutoka Chuo cha Ualimu Morogoro Godfrey Omary amesema anaishukuru Serikali kwa kutoa mafunzo hayo kwa kuwa yanakwenda vikwazo katika vya kiutendaji lakini pia itapunguza utegemezi na hivyo kuongeza ufanisi.

Mafunzo kuhusu matumizi ya TEHAMA na Teknolojia saidizi kwa walimu na wakufunzi na wenye mahitaji maalumu yameanza leo na yanatarajiwa kuhitimishwa  Februari 05, 2020.

Jumamosi, 25 Januari 2020

SHORT TRAINING COURSES SCHOLARSHIP TENABLE IN INDIA FOR THE ACADEMIC YEAR 2019/2020


Call for Application
The General Public is hereby informed that the Government of India through the Indian Technical and Economic Cooperation (ITEC), has granted a full funded scholarship to eligible Tanzanian to pursue Short courses at Indian Public Institutions for the academic year 2019/2020.

A directory of Host Training Institutions and the Training Calendar is available on the website of ITEC through www.itecgoi.in/stream_list.php. Containing a complete list of the Indian Public Institutions as well as specific information about them, including the conditions of access, the course and the duration of the studies. For more information about the programme visit the following link www.itecgoi.in/about.php.

How to apply
1.    Applicants are advised to apply for the current courses as indicated in ITEC training Calendar of 2019/2020;
2.    The applicants after applying online are required to forward the applications to the Embassy/High Commission of India in Tanzania  concurrently accredited for nomination; and
3.    Further, the applicants may later check the status of their applications by logging-in at www.itecgoi.in.

Eligibility
1.    Academic qualifications as laid down by the Institute for the course concerned;
2.    Officials in Government, Public  and Private sectors, Universities,
 Chambers of Commerce and industry, progressive farmers and Research;
3.    Candidate should possess adequate working experience on the related field;
4.    Age limit between 25 to 45 years; and
5.    Medically fit to undertake the training.

Issued by
Permanent Secretary,     
Ministry of Education, Science and Technology,
Mtumba Block,
Afya Street,
P.O.BOX 10,
40479 DODOMA.

Jumanne, 21 Januari 2020

TANGAZO LA KUJIUNGA NA VYUO VYA MAENDELEO YA WANANCHI


Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inatangaza nafasi za kujiunga katika Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi (FDC) kwa mwaka 2020.
Sifa za Mwombaji ni mwananchi yeyote mwenye nia ya kupata ujuzi na maarifa mbalimbali.
Aina ya Mafunzo yanayotolewa ni:
1. MAFUNZO YA UFUNDI STADI- NGAZI YA I, II &III
  1. Ufundi Umeme wa Magari : (Ifakara, Katumba, Nzovwe, Rubondo, Same, Sofi, Kisangwa, Mto wa Mbu,Chala,Handeni, Ikwiriri, Karumo, Kilosa, Katumba, Kibondo, Kilwa Masoko, Kihiga, Mamtukuna, Malampaka, Kiwanda,Malya).
  1. Ufundi Mekanika, (Vyuo vyote vinavyofundisha Ufundi Magari).
  1. Ufundi Umeme wa Majumbani, (Vyuo vyote vinafundisha kozi hii).
  1. Ufundi  Magari : (Bigwa, Chala, Chilala, Handeni, Ifakara, Ikwiririri, Karumo, Kilosa, Kisarawe, Katumba, Kibondo, Kilwa Masoko, Kisangwa, Kihinga, Singida Mamtukuna, Malampaka, Malya, Masasi, Mbinga, Msinga, Mtawanya, Musoma, Mwanhala, Mwanva, Mto wa Mbu, Munguri, Nandembo, Newala, Ngara, Njombe, Nzega, Nzovwe, Rubondo, Same, Sengerema, Sofi, Urambo).
  1. Useremala: (Bariadi, Mtawanya, Chala, Chilala, Chisala, Handeni, Ifakara, Ilula, Ulembwe, Kiwanda).
  1. Uashi: (Vyuo vyote vinavyofundisha Uashi isipokuwa Mtowambu, Nzega, Ikwiriri, Buhangija, Kiwanda, Chilala, Bigwa na Sikonge).
  1. Ushonaji: (Vyuo vyote vinafundisha ushonaji isipokuwa, Arnatouglu, Handeni, Sofi).
  1. Upishi: (Urambo, Sofi, Singida, Same, Nzovw, Nzega, Njombe, Mto wa Mbu, Mwanhala, Mtawanya, Msanginya, Masasi, Mamtukuna, Kiwanda, Kisarawe, Kilosa, Ilula, Ikwiriri, Ifakara, Handeni, Arnatouglu, Bigwa na Bariadi).
  1. Uchomeleaji: (Gera, Ifakara, Karumo, Kisarawe, Kisangwa, Kiwanda, Malya, Mtawanya, Mwanhala, Munguri, Newala, Njombe, Nzovwe, Sikonge, Nzega, Sengerema, Sikonge, Sofi, Ulembwe na Urambo).
  1. Kompyuta: vyuo vyote vinafundisha isipokuwa, (Sofi, Sikonge, Same, Newala, Nandembo, Munguri, Mto wa Mbu, Musoma, Mtawanya, Msingi, Msanginya, Muhukuru, Masasi, Mamtukuna, Kiwanda, Kisangwa, Kisarawe, Ifakara, Handeni, Gera, Chilala na Arnatouglo).
  1. Kilimo na Ufugaji: (Chisalu, Gera, Kiwanda, Handeni, Ifakara, Ikwiriri, Kilosa, Kilwa Masoko, Kisangwa, Mamtukuna, Malampaka, Mamtukuna Malampaka, Malya, Muhukuru, Msanginya, Msingi, Mwanhala, Njombe, Nzovwe, Same, Singida, Bigwa, Tango, Urambo).
  1.  Utunzaji wa watoto (Day care): (Nzovwe, Bigwa, Mtawanya, Msingi, Mtawanya, Msinga, Masasi, Katumba, Chisalu).
  1. Elimu haina mwisho (Sekondari nje ya mfumo rasmi kwa wasichana tu): (Chilala, Ilula, Karumo, Katumba, Malya, Masasi, Muhukuru, Msanginya, Msinga, Msingi, Mtawanya, Mwanva, Mputa, Mto wa Mbu, Ngara, Njombe, Nzega, Nzovwe, Bigwa, Rubondo, Sengerema).
  1. Mpira fursa kwa Wanafunzi wa kike tu: (Sengerema, Nzovwe, Mputa, Masasi, Katumba, Bigwa na Nzega).
  1. Uongozaji Watalii: (Kilwa Masoko, na Ngara).
  1. Udereva: (Tarime, Kiwanda, Tango, Sofi, Sikonge, Rubodo, Nzega, Malya, Kilwa Masoko, Ikwiriri, Chala).
  1. Ufundi Bomba: (Kiwanda).

2. MAFUNZO MAALUM
    Muda hulingana na Mahitaji ya Wahusika
                i.                 Elimu ya Sekondari Nje ya Mfumo Rasmi (Elimu haina Mwisho)
              ii.                  Utunzaji wa Watoto Wadogo (Day Care)
            iii.Mpira fursa (Michezo)

3. MAFUNZO YA MUDA MFUPI
Mafunzo haya hutolewa kwa wananchi mbalimbali sambamba na vikundi mbalimbali kulingana na mahitaji yao.

Aidha, pamoja na mafunzo haya yaliyoainishwa hapo juu, washiriki watajifunza masomo yafuatayo ya Uelewa kulingana na mahitaji ya wahusika. Masomo hayo ni pamoja na: Kiingereza, Uraia, Uchumi, Hifadhi ya Mazingira, Ujasiriamali na Afya ya Jamii.

GHARAMA YA WASHIRIKI
Gharama kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi na Mafunzo Maalum kwa mwanachuo wa Bweni na Kutwa malipo ni kama ifuatavyo:-
a)     Gharama kwa Wanachuo wa Bweni ni shs. 250,000/=

    1. Ada ya Mafunzo                     -TShs.  100,000/=
    2. Gharama nyingine                   -TShs. 150,000/=
Jumla                                        TShs. 250,000/=

NB: Gharama nyingine inajumuisha:

i)   Kitambulisho                                  -TShs      5,000/=
ii)  Fedha ya ukarabati             -TShs.   25,000/=
iii) T-shirt (sare)                      - TShs.   15,000/=
iv) Godoro                               - TShs.     5,000/=
v)  Vifaa vya mafunzo             - TShs    100,000/=


b)    Gharama kwa Wanachuo wa Kutwa ni shs. 245,000/=;

a)     Ada ya Mafunzo                 -TShs.  100, 000/=
b)    Gharama nyingine              -TShs.  145,000
       Jumla                                     -TShs- 245,000/=

NB: Gharama nyingine inajumuisha:

i)   Kitambulisho                    - TShs    5,000/=
ii)  Fedha ya ukarabati            -TShs.  25,000/=
iii) T-shirt (sare)                     - TShs. 15,000/=
iv) Vifaa vya mafunzo           - TShs 100,000/=
                                   - TShs 145,000/=

c)                       Kwa mafunzo ya Muda Mfupi ni Tshs 20,000/= kwa mshiriki kwa mwezi.

N.B - Ada kiasi cha Tshs. 100,000/- ilipwe kwenye mfumo wa Serikali na mwanafunzi atalazimika kupata Namba ya Malipo (Control Number) toka chuoni ili afanye malipo na gharama nyingine zilipwe kwenye akaunti ya Chuo na zitakatiwa risiti ya Chuo.  Ada inaweza kulipwa kwa awamu mbili (2) tu.

Imetolewa na:


KATIBU MKUU
WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA