Jumanne, 26 Septemba 2017

MBINU ZA KUFUNDISHIA ZIMEPUNGUZA UTORO - KKK MKOANI SINGIDA

Walimu wanaofundisha darasa la awali hadi la tatu katika shule ya msingi Nyerere, Mughanga na shule ya wanafunzi wenye mahitaji Maalumu Ikungi zote zilizopo mkoani Singida wameeleza kuwa  mbinu za kuimba, kucheza, kujifunza kwa kushirikisha wanafunzi zinawasaidia wanafunzi kuelewa kwa haraka pamoja na kuwa na umahiri wa  kusoma na kuandika na kuhesabu.

Akizungumza na timu ya wanahabari walio katika ziara ya kufuatilia hali ya ufundishaji na ujifunzaji wa KKK na kuangalia hali ya uboreshaji wa miundombinu mkoani humo Mwalimu Salome Kyomo amepongeza jitihada za serikali za kuwapatia walimu mafunzo ya KKK kwa kuwa mbinu na zana za kufundishia zimeboreshwa.


Kwa upande wake mratibu wa taaluma wa  shule ya msingi Nyerere Lisu Mnyambi amesema shule hiyo ilipokea kiasi cha shilingi Milioni 192 kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia Programu ya Lipa kulingana na matokeo. ambazo zimetumika kujenga vyumba vya madarasa 8, ujenzi wa matundu ya vyoo na hivyo kupunguza  msongamano wa wanafunzi madarasani.

Walimu wa shule ya Msingi Mughanga mkoani Singida  wakiwa kwenye moja ya darasa la Pili ambalo mbinu mbalimbali za kujifunzia na kufundishia , (KKK) zipo katika darasa hilo.


Baadhi ya vyumba vya madarasa katika shule ya msingi Nyerere iliyopo mkoani Singida ambayo imejengwa na fedha zilizotolewa na  Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia Program ya lipa kulingana na Matokeo, (P4R)


Mwanafunzi wa darasa la Pili katika Shule ya Endeberg iliyopo Manyara vijijini akisoma kile kilichoandaliwa na Mwalimu wake huku wanafunzi wengine wakimsikiliza. Lengo la Mwalimu hapo ni kujua wanafunzi wake wanaelewa kile alichowafundisha.

Maoni 1 :