Ijumaa, 19 Januari 2018

Waziri Ndalichako aagiza kusimamishwa kazi kwa Mkuu wa Kitengo Cha Manunuzi cha MUHAS

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof.  Joyce Ndalichako amemuagiza Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Afya na Tiba Shirikishi Muhimbili- MUHAS kumsimamisha kazi Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi wa Chuo hicho.

Waziri Ndalichako amtoa agizo hilo alipofanya ziara katika Chuo hicho jijini Dar es Salaam ambapo amesema Mkuu wa Kitengo hicho Nuru Mkali amekuwa akikuka taratibu za manunuzi na kupelekea kuwepo Kwa ufisadi mkubwa wa fedha za serikali. 

Aidha, amemtaka Mwenyekiti wa baraza la Chuo hicho Mariam Mwafisi kupitia mikataba yote ya manunuzi kwa miaka mitatu ili kuona watu wote walioshiriki katika mchakato huo mbovu wa manunuzi na endapo itabainika basi hatua za kisheria zichukuliwe.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa baraza la Chuo hicho Mariam Mwafisi amesema wamepokea maelekezo na watayafanyia kazi  ikiwemo kumsimamisha kazi Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi.

Akiwa katika  Chuo cha Taaluma na Tiba kilichopo Mloganzila nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam Waziri Ndalichako amemuagiza Makamu Mkuu wa Chuo hicho anaeshughulikia  huduma za Hospitali katika kampasi hiyo Said Abood kuhakikisha anawatembelea  wagonjwa kwa lengo la kutatua changamoto zinazowakabiki pindi wanapokuwa hospitalini hapo.

Prof Ndalichako pamoja na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee  na Watoto  Dkt. Faustine Ndugulile wamefanya ziara katika hositali hiyo ili kujionea changamoto mbalimbali na  namna bora ya kuzipatia ufumbuzi.







Hakuna maoni:

Chapisha Maoni