Ijumaa, 2 Februari 2018

Katibu Mkuu Mkwilapo asisitiza kuzingatiwa kwa taratibu za manunuzi wakati wote wa ukarabati na ujenzi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Dk.Leonard Akwilapo amewataka Wakuu wa Vyuo vya Ualimu, Maboharia na Wahasibu wa Wizara hiyo kuhakikisha wanazingatia taratibu za manunuzi wakati wote wa ukarabati na ujenzi wa Miundombinu ya vyuo  8 vya Ualimu unaotarajiwa kuanza hivi karibuni. 

Dk.Akwilapo amesema hayo leo mkoani Dodoma wakati wa semina Elekezi kwa watendaji hao juu ya namna bora ya kutumia Force Akaunti wakati wa ujenzi kwa kutumia wataalamu na vifaa vyake au kwa  kukodi na kutumia mafundi wengine.

Dk. Akwilapo amewasisitiza wakuu hao wa vyuo vya Ualimu kuhakikisha wanatunza vyema kumbukumbu za matumizi ya fedha, ikiwa ni pamoja na kuunda kamati ambazo zitasimamia manunuzi, upokeaji wa vifaa na matumizi bora ya vifaa hivyo.

Awamu hii ya pili inahusisha Chuo cha Ualimu Patandi, Tarime, Nachingwea, Murutunguru, Mangaka, Tandala, Ilonga na Kinampanda ambapo tayari Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia Programu ya Lipa kulingana na Matokeo imeshatuma fedha za awali   kiasi cha shilingi bilioni 6 kwa ajili kazi hiyo.


Awamu ya kwanza ya ukarabati ilihusisha  Vyuo vya Ualimu 10 ambavyo ni  chuo cha Butimba, Mpwapwa, kleruu, Songea, Kasulu, Tukuyu, Korogwe, Marangu, Morogoro na  Chuo cha Tabora ambapo Wizara ilitumia shilingi Bilioni 10 kwa ajili ya ukarabati wa Vyuo hivyo.






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni