Jumatatu, 16 Aprili 2018

SERIKALI YAAHIDI KUTATUA CHANGAMOTO KWA WANAFUNZI WENYE UZIWI


Waziri wa Elimu, Sayasni na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amekihakikishia Chama cha walimu Viziwi kuwa Serikali iko tayari kusikiliza na kujua changamoto zinazowakabili wanafunzi wenye uziwi ili hatua madhubuti ziweze kuchukuliwa.

Waziri Ndalichako amesema hayo leo mkoani Dodoma alipokutana na kufanya mazungumzo na walimu wenye Uziwi ambapo amewaeleza kuwa hajafurahishwa na matokeo ya kidato cha Nne ya shule ya Sekondari Njombe na kubainisha kuwa ni vyema changamoto zikaainishwa ili hatua ziweze kuchukuliwa.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako  akisalimiana na Mkurugenzi wa Chama cha Walimu wenye uziwi Tanzania Karim Bakari.

Kwa upande wake mratibu wa chama hicho cha Walimu Viziwi Francis Mbisso ameiomba Serikali kutoa semina kwa walimu wanaofundisha wanafunzi Viziwi ili  walimu waweze kuelewa saikolojia ya wanafunzi pale wanapowafundisha, lakini pia kuwe  na wigo mpana  wa mafunzo ya ufundi kwa wanafunzi hao  badala ya kuwalazimisha kusoma masomo ya darasani.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akutana na kufanya mazungumzo na Chama cha Walimu wenye Uziwi Tanzania. Mazungumzo hayo yanalenga kutataua changamoto zinazowakabili wanafunzi wenye uziwi.

Mbisso ameshauri kuwepo kwa mtaala wa lugha ya alama pekee utakaowasiadi wanafunzi wenye uziwi kuelewa kwa uarahisi masomo yao wanapokuwa darasani ikiwa ni pamoja na kuongeza muda ya kipindi darasani ukilinganisha na muda wanaotumia wanafunzi wa kawaida.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Ave Maria Semakafu akisalimiana na Mwalimu Theresia Nkwera mwenye uziwi, ambaye alishiriki majadiliano ya pamoja yenye lengo la kutatua changamoto zinazowakabili wanafunzi wenye uziwi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni