Jumatano, 18 Aprili 2018

WAZIRI NDALICHAKO AZINDUA JENGO LA GHOROFA 10 DIT • AITAKA TAASISI HIYO KUTUNZA MIUNDOMBINU

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako leo amezindua Jengo la kufundishia la ghorofa 10 katika Taasisi ya Teknolojia  Dar es salaam- DIT – Teaching Tower Complex.

Akizungumza mara baada ya kutembelea na kukagua jengo hilo amesema kuzinduliwa kwa jengo hilo kutasaidia kuongeza udahili wa wanafunzi kwa kuwa jengo hilo linauwezo wa kuchukua wanafunzi zaidia ya Mia Tisa kwa mara moja.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako azindua Jengo la ghorofa 10 DIT na ameitaka Taasisi hiyo kutunza miundombinu kwa kuwa imejengwa kwa gharama kubwa na fedha zilizotumika ni za ndani.

Ndalichako amesema kuwa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuondoa upungufu wa kero ya Miundombinu iliyokuwa inaikabili DIT kwa muda mrefu ambapo jengo hilo limeigharimu Serikali zaidi ya Bilioni Tisa ambazo ni fedha za ndani.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akizungumza  na watendaji pamoja na wanafunzi wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam(hawapo pichani) wakati wa kuzindua  Jengo la kufundishia la ghorofa 10.

Kwa upande wake Mkuu wa chuo cha DIT Profesa Preskedis Ndomba ameishukuru Serikali kwa uwekezaji huo  uliofanywa na Serikali ambapo amemhakikishia Waziri wa Elimu kuwa  watailinda miundombinu hiyo ili iweze kutumika kwa muda mrefu kwa lengo la kuongeza tija ya kuwepo kwa wataalamu wa fani mbalimbali hapa nchini


Baadhi ya Watumishi wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam –DIT -wakisikiliza kwa makini hotuba ya Prof Joyce Ndalichako wakati wa kuzindua Jengo la kufundishia la ghorofa 10

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni