Jumamosi, 21 Julai 2018

OLE NASHA AZITAKA TAASISI ZA ELIMU YA JUU KUZINGATIA UBORA WA MAFUNZO WANAYAYOTOA


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha  amezitaka Taasisi za Elimu ya Juu kuzingatia suala la ubora wa mafunzo wanayoyatoa katika programu zao ili kupata wahitimu wenye ujuzi unaotakiwa kwenye uchumi wa viwanda.

Naibu Waziri Ole Nasha amesema hayo Jijini Dar es Salaam wakati wa kufunga   Maonesho ya 13 ya Elimu ya Juu ambapo amesema Serikali ina mategemeo makubwa ya kupata rasilimali watu bora itakayofanya kazi katika viwanda hivyo suala la ubora wa mafunzo linahitaji kupewa kipaumbele.


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Wiliam Ole Nasha akizungumza na wanashiriki (Hawapo pichani) katika maonesho ya kumi na tatu ya Elimu ya Juu wakati wa kufunga wa maonesho hayo katika viwanja vya Mnazi mmoja Jijini Dar es alaam.

“Tunataka mzalishe wahitimu wanaoonekana wamepata Elimu bora na si bora Elimu ambao wataweza kufanya kazi kulingana na mahitaji na matarajio ya taifa letu lakini pia watakaokidhi vigezo na matarajio ya wadau mbalimbali,” Alisisitiza Naibu Waziri Ole Nasha.


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Wiliam Ole Nasha akisikiliza ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali ya elimu  kutoka kwa mmoja wa washiriki wa maonesho ya kumi na tatu ya Elimu ya Juu yanayofanyika jijini Dar es Salaam.

Alisema wizara yake itaendelea kusimamia na kufuatilia kwa karibu zaidi suala la ubora wa Elimu katika ngazi zote na kuzitaka Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) kuhakikisha inafuatiali vyuo kwa karibu ili kuhakikisha wanafuata miongozo iliyopo na kwamba Serikali haitavumilia taasisi au mtu yeyote anayejaribu kukiuka miongozo hiyo kwa sababu yoyote ile.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Wiliam Ole Nasha akikabidhi cheti cha ushiriki kwa mmoja wa wadau wa Elimu ya Juu walioshiriki maonesho ya kumi na tatu ya Elimu ya Juu yanayofanyika jijini Dar es Salaam.
Maonesho ya Elimu ya Juu yamehitimishwa leo na yalikuwa na kauli mbiu ELIMU YA JUU BORA KWA MAPINDUZI YA VIWANDA


Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe Prof. Lughano Kusiluka akijadiliana masula mbalimbali kuhusu Elimu na baadhi ya washiriki wa maonesho ya Elimu Juu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia yaliyofanyika jijini Dar es Salaam 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni