Wathibiti Ubora wa Shule nchini wametakiwa kufanya ufuatiliaji wa karibu
wa taaluma shuleni kwani matokeo bora ya ujifunzaji yanahitaji
usimamizi na tathmini ya mara kwa mara.
Hayo yameelezwa leo mkoani Dodoma na Waziri wa Elimu,
Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako wakati wa hafla ya kukabidhi
magari 45 kwa Wathibiti Ubora wa Shule wa Kanda na Wilaya na magari 2 kwa ajili
ya Baraza la Mitihani Tanzania.
Waziri
wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza wakati wa
hafla ya ugawaji magari kwa Wathibiti Ubora wa Shule Kanda na Wilaya, pamoja na
Baraza la Mitihani la Tanzania. Amesisitiza matumizi bora ya magari hayo ili
yaweze kutimiza lengo lililokusudiwa.
Waziri Ndalichako amesema lengo la Taifa ni
kuwa na watu walioelimika,  mahiri na wabunifu
katika  kuelekea uchumi wa viwanda ifikapo 2025,
hivyo ili kufikia malengo hayo  usimamizi wa karibu na tathmini ya mara
kwa mara inahitajika.
Waziri Ndalichako amewasisitiza Wathibiti Ubora
wa Shule kuhakikisha wanafanya  ufuatiliaji wa karibu wa kitaaluma
ikiwa ni pamoja na kuhakikisha  walimu wanafika
 shuleni  kwa  wakati  wanaingia
 kwenye  vipindi  na wanafundisha.
 “Nataka nione mnasimamia kwa karibu taaluma
na nataka  kuona  mabadiliko makubwa katika shule zetu
za   Serikali  kuanzia  upande  wa  nidhamu na  taaluma ili
mabadiliko yaweze kujitokeza  kwenye Shule zetu,
 na tuone shule
zetu  zinafanya vizuri katika matokeo ya Taifa ya
kidato  cha  Nne,’’ alisisitiza Prof. Ndalichako.
Waziri
wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akikata utepe kama
ishara ya uzinduzi wa magari ambayo ameyagawa kwa Wathibiti Ubora wa Shule ili
kuwawezesha kutekeleza majukumu yao ipasavyo.
Profesa Ndalichako ametaka magari hayo
kutotumika katika malengo yasiyokusudiwa badala yake yatumike tu kwa
ufuatiliaji wa taaluma shuleni. 
“Haya ni magari kwa ajili ya ufuatiliaji wa Elimu, ninaagiza magari haya yasitumike kwa matumizi mengine yoyote tofauti na masuala ya Elimu, naomba
hili
likazingatiwe sana na yeyote atakayekikuka hatua za
kinidhamu  zitachukuliwa,”alisisitiza Waziri Ndalichako.
Waziri
wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akikagua moja ya gari
lililonunuliwa na Wizara kama nyenzo na kitendea kazi kwa Wathibiti Ubora wa  Shule.
Pia Waziri Ndalichako amewataka Wakuu   wa
 Shule  kuendelea  kusimamia  nidhamu  na kutowaonea huruma  wanafunzi wanaokiuka taratibu
za Shule  kwani Serikali haitakuwa  na huruma na
watendaji pale mambo yatakapokuwa hayaendi vizuri. 
“Angalieni  Mkuu wa Shule ya Sekondari Jangwani
ameng’oka  kwa  hiyo  Serikali haitakuwa na huruma nanyi  pale mtakapowalea wanafunzi wenye 
utovu wa nidhamu Shuleni, wanafunzi hawatakiwi kuwa na simu
shuleni  lakini bado wanafunzi wameendelea kuwa na simu,
hakikisheni mnasimamia maadili na nidhamu za wanafunzi kwa mujibu wa taratibu
zinavyoelekeza.
Mapema mwanzoni mwa Mwezi Julai Wizara iligawa pikipiki
2,894  kwa  ajili ya Waratibu Elimu kata ikiwa ni muendelezo wa kutatua changamoto ya usafiri kwaWathibiti Ubora ili wazeze kufikia shule zote na
kufuatilia  hali  ya ufundishaji shuleni.
Baadhi ya Magari ambayo
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imenunua kwa ajili ya Wathibiti Ubora wa
Shule Kanda na Wilaya pamoja na Baraza la Mitihani  Tanzania

 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni
Zingatia: Mwanachama wa blogu hii tu ndiye anayeweza kuchapisha maoni.