Ijumaa, 21 Juni 2019

NDALICHAKO AZINDUA MABARAZA YA UJUZI YA KISEKTA

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amesema serikali kupitia Wizara ya Elimu inaendelea kuimarisha stadi na ujuzi katika sekta sita za kipaumbele ili kufikia azma ya kuwa na uchumi wa kati unaotegemea viwanda ifikapo 2025.

Waziri Ndalichako ametoa kauli hiyo wakati wa halfa ya uzinduzi wa Mabaraza ya Ujuzi ya Kisekta jijini Dar es Salaam ambapo mabaraza hayo yaliyoundwa kupitia Mradi wa Kukuza Ujuzi na Stadi za Kazi (ESPJ) na sekta zilizopewa kipaumbele katika Mpango Mkakati wa Taifa wa Kukuza na Kuendeleza ujuzi ni pamoja na Kilimo, TEHAMA, Nishati, Ujenzi, Uchukuzi na Utalii.

“Katika azma ya Serikali ya kufikia uchumi wa kati unaotegemea viwanda ifikapo 2025, tunapaswa kuhakikisha nchi  yetu inakuwa na nguvukazi yenye ujuzi na stadi stahiki zinazohitajika kwenye soko la ajira,” amesisitiza Waziri Ndalichako.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako, akitoa hotuba yake wakati wa uzinduzi wa Mabaraza ya Ujuzi ya Kisekta uliofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Akizungumzia Mabaraza ya Ujuzi ya Kisekta Prof. Ndalichako amesema Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia iliingia makubaliano rasmi ya ushirikiano (MoU) na Tanzania Private Sector Foundation (TPSF) ili kusimamia uanzishaji na kuratibu mabaraza hayo ambayo yatakuwa kiunganishi muhimu kwa kuwaleta pamoja wadau mbalimbali wa masuala ya kuendeleza na kutumia ujuzi nchini.

“Tutaendelea kutoa ushirikiano kwa sekta binafsi na wadau wengine kwa kuweka mifumo wezeshi na rafiki, programu mbalimbali za kuendeleza ujuzi, na kuimarisha miundombinu ili kuhakikisha nchi inajenga ujuzi na stadi stahiki kwa ustawi wa maendeleo ya nchi,” amesema Prof. Ndalichako.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Salum Shamte, akitoa hotuba ya utangulizi kabla ya kumkaribisha Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako kufungua rasmi Mabaraza ya Ujuzi ya Kisekta.
Waziri Ndalichako amesema kupitia ushirikiano kati ya Sekta Binafsi na Umma serikali inatarajia kupata ushirikiano katika programu za mafunzo ya wahitimu tarajali mahali pa kazi (internships) na kutambua ujuzi uliopatikana nje ya mfumo rasmi wa elimu (recognition to prior learning - RPL) ili kupunguza na kuondoa changamoto mbalimbali zilizopo katika jamii.

Aidha, Prof. Ndalichako ametoa ombi kwa sekta binafsi kuendelea kupokea vijana wanaokwenda kufanya mafunzo kwa vitendo ili kuwajengea utayari wa kuingia kwenye soko la ajira.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako akisalimiana na wadau waliohudhuria katika uzinduzi rasmi wa Mabaraza ya Ujuzi ya Kisekta.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF), Salum Shamte alisema mabaraza yatakuwa ni fursa pekee ya kuunganisha Taasisi Binafsi, Serikali na Wadau mbalimbali wa maendeleo kutoka nje ya nchi katika kuleta ufanisi katika maendeleo.

Shamte amesema TPSF imekuwa ikitoa ushauri na mapendekezo mbalimbali kwa serikali kupitia Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) katika ngazi ya wilaya, Mkoa , Wizara na hata Taifa ili yaweze kufanyiwa kazi.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako, akipongezwa na Mwenyekiti wa Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Salum Shamte mara baada kuzinduzia Mabaraza ya Ujuzi ya Kisekta uliofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa Sekta ya Kilimo akitoa neno la shukrani.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akiwa katika picha ya pamoja na Wawakilishi wa Sekta ya Kilimo.

Wadau wa Sekta ya Nishati wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako.
Wawakilishi kutoka Sekta ya Tehama wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako.

Wawakilishi kutoka TEA na Bodi ya Mikopo wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia akiwa katika picha ya pamoja na Wawakilishi wa wanafunzi wa Vyuo Vikuu.

Washirika wa Maendeleo wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako akiwa katika picha ya pamoja na Wawakilishi wa Sekta ya Utalii.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako akiwa katika picha ya pamoja na Wawakilishi wa Sekta ya Usafirishaji.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni