Jumanne, 11 Februari 2020

WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA KUJENGA KUJENGA BWALO KATIKA SHULE YA MRISHO GAMBO ILIYOPO MKOANI ARUSHA



Akizungumza mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa shule hiyo, Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Leonard Akwilapo  amesema Wizara itajenga bwalo la chakula ili kuwezesha wanafunzi wa shule hiyo kuwa na sehemu nzuri na salama ya kupatia chakula watakapokuwa wakiishi katika mabweni yatakayojengwa na wizara.

"Nimeambiwa wanafunzi wa shule hii wanatoka maeneo ya mbali, Wizara ilishaahidi kujenga mabweni mawili sasa tutajenga na bwalo," amesema Dkt. Akwilapo.

 Aidha, Dkt. Akwilapo amesema  serikali ina wajibu wa kuhakikisha wanafunzi wanasoma  katika
 mazingira salama na yenye miundombinu salama.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo amesema shule hiyo imejengwa baada ya kupokea maombi kutoka kwa  wakazi wa Olasite baada shule yao kuzidiwa na wingi wa wanafunzi.

"Baada ya kupokea maombi kutoka kwa wakazi wa hapa  na kuona kweli kuna shida katika shule hii ya Olasite ndipo tukaanza kutafuta wadau mbalimbali ambao walijitokeza na kusaidia uanzishwaji wa ujenzi wa shule hiyo," amesema Gambo.

Mkuu wa shule hiyo, Fedelis Michael amesema mazingira ya wanafunzi kusoma mbali sana na shule ni changamoto kwao kwani njiani wanakutana na mambo mengi ambayo yanaweza kuwasababishia kushindwa kusoma vizuri.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni