Jumatano, 12 Septemba 2018

WIZARA YA ELIMU YAWAJENGEA UWEZO WABUNGE WA KAMATI YA BUNGE YA HUDUMA NA MAENDELEO YA JAMII KUHUSU MAJUKUMU YANAYOTEKELEZWA NA WIZARA HIYO


Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknlojia leo imewajengea uwezo Wabunge wa Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa kuwasilisha majukumu 14 yanayotekelezwa na Wizara hiyo kwa mujibu wa hati idhini iliyotolewa April 22, 2016.

Akiwasilisha majukumu hayo Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango Makuru Petro ametaja majukumu hayo kuwa ni pamoja na kutunga na kutekeleza Sera za Elimu, utafiti, Huduma za Maktaba, Sayansi na Teknolojia na uendelezaji wa mafunzo ya Ufundi, kuendeleza Elimu kwa kutoa ithibati ya mafunzo ya Ualimu na Maendeleo ya kitaalamu ya Walimu, Kusimamia uendelezaji wa mafunzo katika vyuo vya Maendeleo ya wananchi, na kusimamia mfumo wa tuzo wa Taifa.
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo akifafanua jambo kuhusu majukumu yanayotekelezwa na Wizara hiyo wakati wa kikao cha pamoja na Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii mkoani Dodoma.

Majukumu mengine ni kuainisha mahitaji ya nchi katika ujuzi, kuweka viwango vya Taaluma ya Ualimu ikiwemo kuanzisha bodi ya kitaalamu ya walimu, kusimami ithibati na uthibiti ubora wa shule kwa kuweka viwango, kusimamia Huduma za machapisho ya kielimu ikiwemo mitaala na vitabu, kuimarisha utumiaji wa Sayansi, Teknolojia na hisabati, kuendeleza wataalamu wa ndani katika Sayansi na Teknolojia, kuratibu na kusimamia utafiti, ubunifu katika fani za Sayansi na Teknolojia, kusimamia Tume ya Taifa ya UNESCO, uendelezaji wa Rasilimali watu na kuratibu shughuli za Idara, mashirika, wakala, programu na miradi iliyo chini ya Wizara.
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) Dkt. Aneth Komba akiwasilisha utekelezaji wa majukumu ya Taasisi hiyo wakati wa kikao na  Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii wakati wa kikao cha pamoja kilichofanyika mkoani Dodoma.

Kupitia uwasilishaji wa majukumu hayo ya Wizara wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo walipata fursa ya kujibu maswali mbalimbali yaliyoulizwa na Wabunge kwa lengo la kupata uelewa.

Baadhi ya Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wakishiriki kikao cha pamoja na Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kilichofanyika mkoani Dodoma
Taasisi zilizoshiriki katika kujibu maswali mbalimbali ya Wabunge ni pamoja na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi, (NACTE), Tume ya vyuo Vikuu Tanzania, (TCU), Taaaisi ya Elimu Tanzania (TET).
1.      Baadhi ya Watendaji wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wakishiriki kikao cha pamoja na Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kilichofanyika mkoani Dodoma

Jumamosi, 8 Septemba 2018

WAZIRI NDALICHAKO ASEMA SERIKALI IKO TAYARI KUSHIRIKIANA NA TAASISI BINAFSI


Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Profesa , Joyce Ndalichako amesema  serikali iko tayari kuendelea kutoa ushirikiano katika Taasisi binafsi ambazo zimeendelea kutoa mchango mkubwa katika sekta ya Elimu hapa nchini.

Waziri Ndalichako amesema hayo mkoani Dodoma wakati akizindua jengo la shule ya Msingi Misercodia inayomilikiwa na kanisa katoliki Shirika la Watawa wa Misericordia.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako wkiwa na Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda wakati wa uzinduzi wa  Jengo la Shule ya Msingi Misercordia Mkoani Dodoma

Waziri Ndalichako amesema Serikali imekuwa ikitambua na kuheshimu kazi kubwa inayofanywa na kanisa hilo katika kusaidia ujenzi wa miundombinu kwenye sekta ya Afya na Elimu hapa nchini na ikiwa ni pamoja na  kutatua changamoto mbalimbali kwa wakati.

"Wakati nakuja kuzindua shule hii  nilimtaarifu Mheshimiwa Rais Dkt. John Magufuli na ametuma salamu, amesema niwaambie anawashukuru sana Maaskofu na Watawa kwa kuwa  mnaunga mkono juhudi za Serikali katika  ushiriki wa miradi mbalimbali ya maendelea kwa vitendo,”amesema Waziri Ndalichako.
Waziri akiwa aa Watawa wakati wa kuzindua Shule ya Kanisa ya Misercordia iliyopo Mkoani Dodoma ambapo Serikali imesema iko tayari kushirikiana na Taasisi Binafsi katika maendeleo.

Waziri huyo wa Elimu amesema , ujenzi wa Miundombinu hiyo umekuja wakati muafaka ambapo uhitaji wa shule za mchepuo wa kingereza ni mkubwa , kutokana na watumishi wengi wa serikali kuhamia Dodoma na hivyo kuhitaji shule kwa ajili ya watoto wao.

Kuhusu malezi ya wazazi, Waziri amesema hivi sasa wazazi wamesahau majukumu yao na badala yake wamekuwa wakifanya kazi zote ambazo zilipaswa kufanywa na watoto jambo ambalo sio sawa kwani wanajenga taifa la wavivu.


Wanafunzi na Walimu wa Shule hiyo ya Misercordia wakati wa uzinduzi wa Jengo la gorofa katika shule hiyo.

Waziri Ndalichako pia amezipongeza shule  nyingine za dini kwa kusimamia maadili kwa wanafunzi, ambapo ametumia  nafasi hiyo kuwakaribisha wawekezaji kuja kuwekeza kwa kujenga miundombinu ya shule za msingi na sekondari kwani hivi sasa Dodoma inauhitaji mkubwa wa shule kwa sasa.

Waziri Ndalichako ameipongeza shule kwa kufanya vizuri katika matokeo ya kidato Cha Nne na Sita na kuongoza kitaifa katika somo la kiingereza, pia amezipongeza shule nyingine za dini kwa kusimamia maadili kwa wanafunzi.


Uzinduzi Jengo la   Shule ya Misercordia, iliyopo Mkoani Dodoma uzinduzi huo umefanywa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknlojia Prof. Joyce Ndalichako ambapo Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda pia alishiriki shughuli hiyo.

Alhamisi, 6 Septemba 2018

ALIYOYASEMA WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA PROF. JOYCE NDALICHAKO LEO WAKATI WA MAHOJIANO NA TBC TAIFA KUHUSU MUSWADA WA SHERIA YA BODI YA KITAALAMU YA WALIMU


- Lengo la Bodi ni kuwa na Muundo na Chombo Cha Kisheria ili kutambua rasmi taaluma ya Ualimu kama zilivyo taaluma nyingine

- Ili kutimiza malengo yaliyowekwa na Serikali katika Elimu, thamani ya walimu ni jambo ambalo linapewa kipaumbele sana.

-Muswada wa Sheria ya bodi ya kitaalamu ya walimu umekuwa shirikishi katika hatua zote ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha Walimu,Maafisa Elimu wa Wilaya, Mikoa,Wathibiti Ubora,Chama Cha Walimu Tanzania,Taasisi mbalimbali na Wizara ikiwemo ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI).

- Wadau wengine walioshirikishwa Kuanzia hatua za awali ni pamoja na Haki Elimu, CHAKAMWAKA, TAPIE, TAMONGSCO na Mtandao wa Elimu Tanzania(TEN/MET)

- Malengo ya Bodi hii ya walimu hayafanani na chombo kingine, vyama vingine vinaangalia maslahi ya walimu wakati bodi inaenda kuleta hadhi kwa kutambua walimu wote waliopo na wasiokuwepo madarasani.

-Tume ya Utumishi wa walimu imejikita katika utumishi kwa maana ya kuangalia orodha ya walimu walioajiriwa na serikali na uratibu wa masomo wakati bodi itaangalia mabadiliko mbalimbali katika dunia ikiwa ni pamoja na kuangalia nafasi za kuwaendeleza walimu.

-Bodi pia itasimamia vigezo kwa kuhakikisha mwalimu lazima awe amehitimu katika Chuo kinachotoa mafunzo, pia bodi itasimamia suala la maadili kwa walimu.

-Bodi ya kitaalamu ya walimu itakuwa na jukumu la kupokea malalamiko, kuchambua na kuyapatia ufumbuzi malalamiko ya Walimu wachache ambao wamekuwa wakifanya matendo ambayo ni kinyume na maadili ya Ualimu.

-Bodi itatoa fursa kwa walimu kujadili kwa kina masuala yao ya kitaalamu kwa lengo la kuyapatia ufumbuzi.

-Waziri Ndalichako pia amelaani vikali vitendo vinavyofanywa na baadhi ya walimu vya kutoa adhabu kwa wanafunzi na ameonya walimu kuacha kumalizia hasira zao kwa wanafunzi.

-Waziri amesema uchapaji  hovyo  wa viboko kwa wanafunzi ni kinyume na taratibu za Wizara, sasa kuwepo kwa Bodi ya kitaalamu itahakikisha inawabana walimu watakaokwenda kinyume na taratibu.

- Waziri amewataka walimu kuacha mara moja tabia za kuchapa wanafunzi hovyo na badala yake wawapende watoto na wahakikishe wanawasidia katika kuwakuza kwenye maadili na malezi yanayokubalika kwenye Taifa.

Jumanne, 4 Septemba 2018

RAIS MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA CHUO CHA UALIMU MURUTUNGURU


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt John Magufuli leo ameweka jiwe la msingi kwa ajili ya upanuzi wa Chuo Cha Ualimu Murutunguru, kilichopo Wilayani Ukerewe mkoani Mwanza.

Rais Magufuli amesema Chuo Cha Murutunguru kwa sasa walimu wanaohitimu ni ngazi ya cheti, lengo la serikali ni kianze kutoa ngazi ya Diploma na baadae kikiongezewa miundombinu kiweze kutoa shahada.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. John Pombe Magufuli akiweka Jiwe la Msingi katika Chuo cha Ualimu Murutunguru Wilayani Ukerewe mkoani Mwanza ambapo amewapongeza Viongozi wa Wizara ya Elimu kwa kusimamia vizuri miradi inayotekelezwa na Wizara hiyo.

Rais Magfuli pia amewapongeza Viongozi wa Wizara ya Elimu kwa kusimamia vizuri miradi inayotekelezwa na Wizara hiyo.

Pia Rais amewashukuru  washirika wa Maendeleo hususan nchi ya Uingereza kwa kuendelea kufadhili miradi ya Elimu.
Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wakishuhudia uwekaji wa jiwe la Msingi kwa ajili ya upanuzi wa Chuo cha Ualimu Murutunguru kilichopo Wilaya ya Ukerewe Mkoani Mwanza. 

Upanuzi wa ujenzi wa Chuo hicho unahusisha jengo la Utawala, vyumba vya madarasa, bwalo la Chakula, hosteli za wanafunzi, jengo maalumu la kupokelea umeme na ujenzi wa mifumo ya Maji na umeme.
Muda mfupi baada ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako kumpokea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. John Pombe Magufuli kwa ajili ya kuweka Jiwe la Msingi la upanuzi wa Chuo cha Ualimu Murutunguru. 

Ujenzi huo utagharimu takriban bilioni mbili nukta Tatu na inatarajia kukamilika oktoba mwaka huu.
Muonekano wa vyumba vya madarasa katika Chuo cha Ualimu Murutunguru, ambapo leo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. John Pombe Magufuli ameweka jiwe la msingi ambalo linahusisha ujenzi wa Jengo la utawala, bwalo la chakula, hosteli za wanafunzi, jengo maalum la kupokelea umeme na ujenzi wa mifumo ya maji na umeme.  

Ijumaa, 31 Agosti 2018

KATIBU MKUU WIZARA YA ELIMU AWATAKA WAKUU WA VYUO VYA UALIMU KUFUATA TARATIBU KATIKA UTENDAJI


Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo amewataka Wakuu wa Vyuo vya Ualimu vya Serikali kuacha kufanya kazi kwa mazoea badala yake wafuate taratibu wakati wa kutekeleza majukumu yao ya kikazi ikiwa ni pamoja na kushirikisha watumishi na wanafunzi wa Chuo taarifa za mapato na matumizi ya fedha.

Dk. Akwilapo ameyasema hayo leo Jijini Dodoma wakati alipokutana na Wakuuu wa Vyuo hivyo kwa lengo la kujadili mafanikio, changamoto na mikakati waliyonayo katika kuhakikisha majukumu na uendeshaji wa vyuo yanatekelezeka bila changamoto ili waweze kufikia azma ya kuandaa walimu bora.
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo akizungumza na Wakuu wa Vyuo vya Ualimu vya Serikali (hawapo pichani) katika kikao kazi cha kujadili mafanikio, changamoto na Mikakati bora ya kuwezesha Vyuo  kutekeleza majukumu yake bila changamoto Mkoani Dodoma. 

Pia Katibu Mkuu huyo amewataka Wakuu wa Vyuo kuwasirikisha wale wanaowasimamia katika kuandaa mikakati ya utendaji ili waweze kutoa mchango katika kutekeleza mikakati hiyo na kufikia malengo mapana ya Wizara ambayo ni kutoa Elimu bora.

Katika hatua nyingine Dk. Akwilapo amewataka Wakuu wa Vyuo hao kuanisha mahitaji ya rasilimali watu ambayo inahitajika vyuoni inayoendana na kozi zinazofundishwa katika Chuo husika ili kuepuka kuwa na rasilimaliwatu isiyoendana na mahitaji ya Chuo. 
Baadhi ya Wakuu wa Vyuo wakifuatilia maelekezo ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo wakati wa kikao cha pamoja kilichofanyika leo  Agosti 31, 2018 katika Chuo Kikuu cha Dodoma Jijini Dodoma.  

Naye Mwenyekiti wa Wakuu wa Vyuo vya Ualimu vya Serikali ambaye pia ni Mkuu wa Chuo cha Ualimu Morogoro Agustine Sahili amesema wanaishukuru Wizara kwa kuandaa vikao vya aina hiyo kwani vinawasaidia kuwakumbishia taratibu za kazi na kuahidi kutekeleza yale yote waliyoagizwa ili kuimarisha utendaji katika maeneo ya kazi.

Kikao kazi hicho kimeshirikisha Wakuu wa Vyuo vya Ualimu vya Serikali 35 vilivyopo hapa nchini.
Wakuu wa Vyuo vya Ualimu vya Serikali wakiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo 

PROF. MDOE AITAKA ESPJ KUACHA ALAMA NA KUTEKELEZWA KATIKA MUDA ULIOPANGWA


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa James Mdoe ameutaka Mradi wa Kukuza Ujuzi na Stadi za Kazi kwa lengo la kuzalisha ajira (ESPJ) kuhakikisha inatekeleza vizuri malengo ya mradi yaliyokusudiwa ikiwa ni pamoja na kuonyesha thamani ya fedha ili Taifa liweze kufikia malengo ya nchi ya kufikia uchumi wa viwanda hadi ifikapo mwaka 2025.

Profesa mdoe ametoa maagizo hayo mkoani Morogoro wakati wa kikao kazi cha waratibu wanaohusika na mradi wa ESPJ kutoka kwenye Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na sekta binafsi na kusisitiza kuwa mradi huo unatakiwa kufanya mambo ambayo yataacha alama ikiwa ni pamoja na  kuhakikisha unafanyika katika muda uliopangwa.

“Bado tuko nyuma katika utekelezaji, wadau na viongozi wanajiuliza umuhimu wa huu mradi, sasa tutekeleze vizuri mradi  ili thamani ya fedha ionekane. Mradi huu upo kwenye moyo wangu nitafurahi kuona unaacha alama na katika kujifunza tuangalie namna mradi wa EP4R ulivyoacha alama, sasa ESPJ na yenyewe ifanye hivyo hivyo,”amesema Profesa Mdoe.
Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa James Mdoe akizungumza na Waratibu wa Mradi wa Kukuza ujuzi na Stadi za Kazi kwa lengo la kuzalisha ajira (ESPJ), hawapo pichani ambapo ameutaka mradi huo utekelezwe na uwe na matokeo chanya.

Naibu Katibu Mkuu huyo pia amesema kuwa kiuhalisia mradi umechelewa kuanza sasa katika kuutekeleza lazima umakini uwepo ili matokeo chanya ya mradi huo yaweze kuonekana.

Kikao kazi hicho kinahusu uwasilishaji wa  ripoti mbalimbali zinazohusu utekelezaji wa mradi , ikiwa ni pamoja na kufanyika majadiliano ya pamoja kwa lengo la kujengeana uwezo kutoka Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Elimu, Idara ya Elimu ya juu, Kitengo cha Sheria, Idara ya Sera na Mipango, mratibu kutoka ofisi ya TPSF, pamoja na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.
Waratibu wa Mradi wa Kukuza ujuzi na Stadi za Kazi kwa lengo la kuzalisha ajira (ESPJ) wakiwa katika kikao kazi cha kujengeana uwezo mara baada ya kuwasilishwa kwa ripoti mbalimbali kuhusu utekelezaji wa mradi huo. Kikao hicho kinafanyika kwa siku mbili, Agosti 31 mpaka Septemba 1 mkoani Morogoro.


MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY

SCHOLARSHIP TENABLE IN BRAZIL FOR THE ACADEMIC YEAR 2018/2019
Call for Application
The General Public is hereby informed that, the Republic of Brazil under the Coordination of the Improvement of Higher Education Personnel (CAPES) is offering PhD Scholarships to Tanzanian Citizen.  Successful candidates will be required to pursue their studies in various public higher learning institutions in Brazil for the academic year 2018/2019.  For more information the modes of application and other requirements please follow the provided links.
Mode of Application

All Applicants are requested to complete application online on http://www.inscricao.copess.gov.br/individual.

Through which you will find link that will guide you to register and fill application form and upload all documents required and finally submit online.

The following are the documents required to be uploaded as attachments:-

i                      Page of your Passport;
ii                   Birth Certificate ;
iii                 Academic Certificates ;
iv                 Academic Transcripts;

NB: Detailed information regarding the Scholarships can be accessed from the following webpage: http://www.inscricao.copess.gov.br/individual/cooperacao
International/multinational/pec-pg
This is issued by




Permanent Secretary
Ministry of Education, Science and Technology
University of Dodoma
College of Business and Law
Block 10
P .O. Box 10
40479 Dodoma.
Deadline for applications is 31th August, 2018