Jumanne, 2 Oktoba 2018

KATIBU MKUU WIZARA YA ELIMU AMEWATAKA WATENDAJI KUZINGATIA SHERIA KATIKA KUSIMAMIA MIRADI YA SERIKALI


Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo amewataka washiriki wa mafunzo ya Force Akaunti kuhakikisha wanazingatia Kanuni, taratibu na Sheria wakati wa usimamiaji wa ujenzi na ukarabati  wa miradi ya serikali.

Dkt. Akwilapo ametoa kauli hiyo wakati akifunga mafunzo ya siku mbili ya matumizi ya Force Akaunti yanayofanyika mkoani Morogoro ambayo yameshirikisha  watumishi wa Serikali wakiwemo Wakurugenzi wa Halmashauri, Wakurugenzi wa kanda VETA, Maafisa Kutoka  Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Maafisa kutoka VETA.



Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo amefunga mafunzo ya Force Akaunti ambapo pia amewataka watendaji kuzingatia taratibu,kanuni na sheria za Fedha.
Katibu Mkuu huyo amewaeleza washiriki hao kuwa utaratibu wa Force Akaunti upo kisheria, hivyo amewasisitiza washiriki kuhakikisha wanakuwa na utunzaji wa kumbukumbu ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa risiti za kielektroniki (EFD).



Dkt. Akwilapo  amesema kuwa Force Akaunti ikisimamiwa vizuri inaonyesha thamani ya Fedha, mradi unakamilika na kuwa yote hayo yanawezekana enadapo  ushirikiahwaji na uwazi miongoni mwa Jamii utakuwepo katika eneo ambalo mradi unatekelezwa.


Washiriki wakifuatilia mafunzo ya Force Akaunti yenye lengo la kuwajengea uwezo washiriki namna bora ya kusimamia miradi ya ujenzi na ukarabati yanayofanyika Mkoani Morogoro.
Mafunzo hayo ya siku mbili yanaratibiwa na mradi wa kukuza Maarifa, Stadi na ujuzi (ESPJ) yamehusisha Wakurugenzi wa halmashauri za Kasulu,Ngorongoro,Kongwa,Nyasa, Wakurugenzi wa  Kanda VETA, Wakurugenzi wasaidizi kutoka Makao Makuu VETA na Maafisa kutoka VETA.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo akisindikizwa  na Mkurugenzi wa Elimu ya Ufundi Dkt. Noel Mbonde pamoja na mratibu wa mafunzo ya kukuza maarifa, stadi na Ujuzi (ESPJ), Dkt. Keneth Hosea baada ya kufunga mafunzo ya Force Akaunti yaliyofanyika mkoani Morogoro.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni